• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Wasimamizi wa huduma za afya watakiwa kuimarisha mifumo ya uwajibikaji

Imewekwa tar.: March 17th, 2019


Naibu Katibu Mkuu Afya, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt. Dorothy Gwajima amewagiza waratibu wa timu za usimamizi huduma za afya Mikoa (RHMT) na Halmashauri (CHMT) nchini kuhakikisha, wameimarisha mifumo ya uwajibikaji ili kuleta mabadiliko katika sekta ya afya nchini.

Ameyasema hayo alipokuwa kwenye mwendelezo wa ziara zake za kikazi kwa lengo la kukagua uwajibikaji wa timu hizi kwa Mkoa wa Dodoma katika kituo cha afya cha Bahi kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma.

Dkt. Gwajima amesema, zoezi la kuwapima uwajibikaji limeanzia Mkoani Dodoma likiwa ni endelevu ambapo ndani ya siku 90 litakuwa limekamilika nchi nzima ambapo wale wote wasiopenda kubadilika watapangiwa majukumu mengine wanayoyamudu.

“Hakuna haja ya kila siku semina, washa, mikutano halafu ukienda vituoni, mambo ya kawaida kabisa unakuta hayako vizuri wala takwimu hakuna na hakuna maelezo yoyote yenye mashiko kwa nini hali imekuwa hivyo ilivyo” Amesema Dkt. Gwajima.

Dkt. Gwajima amesema, pamoja na kazi nzuri zinazofanywa katika baadhi ya maeneo, yapo masuala ya msingi ambayo, yanahitaji kusimamiwa vizuri zaidi na na   hayahitaji chochote cha ziada zaidi ya uwajibikaji imara wa viongozi waliopewa dhamana.

Dkt. Gwajima amesema, Serikali haitavumilia kuwa na waratibu ambao, hawaleti msukumo katika kuleta mabadiliko ya uwajibikaji na badala yake wamebaki kusafiri na kuhudhuria semina, washa na mikutano ambayo haileti tija katika maeneo yao ya kazi.

“Inasikitisha kuona baadhi ya waratibu wanahudhuria semina, mikutano na warsha mbalimbali lakini hakuna mabadiliko na wengine hukaa ofisini na hata wanapoenda kutembelea vituo hawaoni mapungufu na wakiyaona hawaandai mpangokazi wa kuboresha na wakiandaa mpangokazi hawafanyi ufuatiliaji bali, wanafungia taarifa kwenye makabatikatika utendaji kazi wa sasa” Anafafanua Dkt. Gwajima.

Aidha, amesema waratibu ambao wanashindwa kwenda na kasi ya usimamizi unaotakiwa enzi hizi, wajipime mapema kabla ya kupimwa na tayari mpaka sasa  Dkt. Gwajima amewabadilisha waratibu kadhaa katika ziara zake baada ya kuona hawasimamii wajibu wao wa msingi bali wanajitetea zaidi kuliko kuonesha njia hata pale ambapo, hapahitaji fedha bali uwajibikaji tu.

“Wakati wa kusema bila takwimu umeisha. Kama umeingia kazini lazima useme umefanya nini? Kama ni wateja je, umehudumia wangapi siyo kulalamika tu watumishi hawatoshi, je umehudumia wateteja wengi kiasi gani kuzidi uwingi wa majukumu uliyowekewa kwa vigezo na takwimu? Uchache wa watumishi siyo namba bali ni sambamba na uwingi wa majukumu kwa takwimu zisizotia shaka.” Amesema  Dkt. Gwajima

Dkt. Gwajima ameawaagiza waratibu kufanya usimamizi na ufuatiliaji  kwa weledi mkubwa ambapo kila mmoja atatakiwa kuonyesha ameona nini na mpangokazi ni upi na umefanikisha ufumbuzi wa changamoto ngapi, kama umekwama je, umechukua hatua gani za kuomba msaada.

Kuhusu ushirikishwaji wa wadau Dkt. Gwajima amezielekeza timu hizo kuwa na  Kamati za Afya za Vituo na Bodi za Afya ambazo, ni wawakilishi wa wananchi ziwezeshwe ili, kuimarisha kiungo kati ya kituo na wananchi wanaowakilishwa na Kamati hizi. Bila kiungo hiki muhimu kati ya vituo na wananchi ni dhahiri kuwa, tutakwama kwenda na kasi tunayohitaji.

Ametoa wito kwa timu za afya nchini kujifunza toka timu za Dodoma ambao, kwa kutumia fursa ya kuwa karibu na Wizara wameona kwa vitendo nini kinatakiwa ili, nao waanze mara moja kuimarisha mifumo na kuanza mbio za mabadiliko kabla zoezi la tathmini ya Wizara halijawafikia hivyo RHMT na CHMT zinahitajika kuwa imara ili, kuchochea huduma bora katika vituo vya tiba.

Dkt.Gwajima ameendelea kusisitiza kuwa, ni wakati wa kila aliyepewa dhamana kuvaa koti la uzalendo na kuakisi kwa vitendo mwendo wa Serikali ya awamu ya tano katika kuleta mabadiliko ya uwajibikaji kwa haraka.

Aidha, amewapongeza watumishi wote ambao, pamoja na changamoto ambazo zipo, wameendelea kupambana na kuleta mabadiliko na amewaasa kutokatishwa tamaa na wachache wasiopenda kubadilika maana, Serikali ina macho na Jamii pia ina macho na inatambua juhudi za kila mmoja na haitawavumilia wale ambao, wanarudisha nyuma kasi ya maendeleo.

Aidha ikumbukwe kuwa  Dkt.Gwajima ameendelea kufanya ziara zake za kikazi za kukagua utendaji kazi wa vituo vya huduma za afya katika  Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya  Chamwino na Halmashauri ya  Wilaya Bahi na itahitimishwa kwa  kuwa na kikao cha Wadau wote ili, kwa pamoja kujionea hali halisi ilivyo na kuwekeana mikataba ya kazi na uwajibikaji.




Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.