Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wananchi wa kikombo waipongeza Serikali kwa kuanzisha kliniki tembezi

Imewekwa tar.: August 16th, 2019

Wananchi wa Kijiji cha Kikombo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuanzisha huduma ya kiliniki tembezi ambayo inatoa huduma za afya karibu na maeneo wanayoishi jamii.

Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata ya Kikombo Mhe. Yona Kusaja wakati wa uzinduzi wa kiliniki tembezi uliyofanyika leo katika Kituo cha afya Kikombo kilichopo katika Kijiji cha Kikombo, Kata ya Kikombo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mhe. Kusaja amesema kuwa ujio wa kiliniki tembezi umesaidia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa wataalam waliobobea katika magonjwa mbalimbali hivyo kuwafanya wananchi  wengi  kujitokeza  kwa ajili ya kufanyiwa vipimo  na kupatiwa  tiba kwa haraka na wakati kwa gharama nafuu.

“Wazee wengi wamejitokeza kuja kuchunguzwa afya zao jambo ambalo linatia moyo, kutokana na huduma hizo kusogezwa karibu na wananchi na wanatumia gharama ndogo kutibiwa” Amesisitiza Mhe. Kusaja.

Akizindua Kiliniki hiyo Tembezi Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi amewaomba wananchi kutokuwakatisha tamaa watoa huduma za afya nchini bali wawatie moyo kwa kuwa wanafanyakazi ngumu ya kuokoa jamii hivyo hawana budi kuwaombea na kuwajali watumishi hao.

“Watumishi wa kada ya Afya wanafanyakazi katika mazingira magumu ya kuwahudumia wagonjwa na kuficha siri zao, hivyo ifike wakati wananchi watambue kuwa kazi hiyo ni ya kujitolea hivyo tuwatie moyo na kuwaombea kwa mwenyezi mungu” Amesisitiza Mhe. Katambi

Mhe. Katambi amewataka watumishi wa afya kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma wa kuwajali na kuwahudumia wananchi kwa upendo ili waweze kuvutiwa na huduma zinazotolewa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Amesema kuwa ni wajibu wa watoa huduma za afya nchini kuhakikisha wanatoa huduma bora za afya  na zenye viwango kwa jamii ili kupunguza malalamiko katika Sekta ya Afya nchini.

Wakati huohuo  Afisa Ustawi wa Jamii Bi. Shekilaga Nkinda kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (ambaye pia ni Mlezi wa Timu za Afya Mkoa wa Dodoma) amewaomba wananchi kuhakikisha wanakitumia kituo cha afya cha Kikombo kwa kuwa ni mali yao na kimejengwa kwa ajili ya kuwapatia huduma bora za afya.

Amesema kuwa inasikitisha kuona kuwa kituo kimejengwa kwa gharama kubwa na Serikali lakini bado wananchi wanaenda kupata huduma hizo katika kituo cha afya cha Chamwino na Hospitali ya Mkoa wa Dodoma jambo ambalo halileti picha nzuri kwa jamii.

“Serikali imetumia gharama kubwa kujenga miundombinu ya kituo hichi cha afya lakini inashangaza kwa mwezi mmoja ni wakina mama 30 tu ndio waliokuja kujifungua hapa, ninawaomba wananchi mkitumie kituo chenu “ Anasisitiza Nkinda

Bi. Nkinda amewaomba wananchi kuhakikisha wanalinda miundombinu ya kituo hicho na pia wanatoa taarifa kwa viongozi pale wanapoona huduma zinazotolewa katika kituo hicho zipo nchi ya viwango vinavyohitajika.

Amewaomba wananchi kuhakikisha wanajiunga na bima ya afya ili waweze kupata huduma za afya kwa urahisi pale wanapokuwa hawana fedha.

Hata hivyo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Gatete Mwihava amesema kuwa wamebuni huduma ya kiliniki tembezi ili iweze kuwasaidia wananchi maskini kwa kuwaletea wataalam wa magonjwa mbalimbali ili kuwapunguzia gharama za kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo.

Amesema huduma ya kliniki tembezi inawataalam wa macho, meno, wataalam wa afya ya mama na mtoto, magonjwa yasiyoambukizwa, saratani ya kizazi na matiti, na hivyo huduma hiyo itaendelea kutelewa katika Halmashauri zote za Jiji la Dodoma.

Aidha, ikumbukwe kuwa, Ofisi ya Rais TAMISEMI ilishatoa maelekezo kwa Timu za Afya Mikoa na Halmashauri nchi nzima kwamba, wahakikishe wanazingatia kuanzisha huduma za Kliniki Tembezi ili, kuwapunguzia mzigo wananchi kufuata huduma mbali na makazi yao.

Na. Angela Msimbira KIKOMBO



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.