Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Wakurugenzi wa Halmashauri watakiwa kutenga fedha za kutokomeza mazalia ya mbu.

Imewekwa tar.: October 23rd, 2019

Wakurugenzi wa Halmashauri watakiwa kutenga fedha za kutokomeza mazalia ya mbu.

Na Mathew Kwembe

Wakurugenzi wa Halmashauri wametakiwa kutenga fedha katika mipango ya bajeti za halmashauri zao kwa ajili kununulia dawa ya kupulizia wadudu wanaosababisha magonjwa mbalimbali nchini ukiwemo ugonjwa wa malaria, kama mkakati mmojawapo wa kuhakikisha kuwa Tanzania inatokomeza ugonjwa huo nchini kutoka maambukizo ya asilimia 7.3 hivi sasa hadi asilimia 1 ifikapo mwaka 2030.

Sambamba na hilo, Wakurugenzi wa halmashauri wametakiwa kulipa madeni yao baada ya kuchukua dawa za kupulizia wadudu katika kiwanda cha kutengeneza dawa hizo kilichopo kibaha, mkoani Pwani.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dkt Dorothy Gwajima mara baada ya kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa wadau wanaohusika katika kudhibiti na kutokomeza ugonjwa wa malaria nchini.

Amesema hatarajii katika bajeti zijazo, kuona halmashauri hazitengi fedha kwa ajili ya kudhibiti na kutokomeza mazalia ya mbu katika halmashauri zao kwani hazitapita.

“Haitapita bajeti ya halmashauri kama haitaweka mikakati ya kudhibiti Malaria sambamba na maelekezo tuliyokuwa tukiyapeleka na mafunzo ambayo tumekuwa tukiyatoa,” amefafanua.

Dkt Gwajima ameongeza kuwa ni muhimu fedha hizo zitengwe ili zitumike katika kutokomeza mazalia ya mbu kwani wataalamu wa halmashauri wanajua ni maeneo gani ya halmashauri yenye mazalia mengi ya mbu wanaoambukiza ugonjwa wa malaria.

“Kwa hiyo lazima ionekane pale ni kiasi gani cha dawa kitaagizwa kutoka katika kiwanda chetu cha kibaha kinachozalisha dawa zinazotumika kupulizia kwenye mazalia ili kudhibiti ongezeko la wadudu hawa,” amesema na kuongeza:

“Wakurugenzi hawa walichukua hizi dawa kibaha hawajalipa, kwanza walipe deni, kisha wapange kwenye bajeti zao kuhakikisha kuwa kazi hiyo inafanyika.”

Amesema kuwa ni jukumu la wataalamu kuainisha maeneo yenye mazalia mengi ya mbu ili dawa zitakazonunuliwa ziweze kutumika vizuri, badala ya kupuliza kila eneo.

Amesema kuna maeneo kwenye halmashauri ambayo yanajulikana kabisa ndiyo yenye mazalia ya mbu na kwamba dawa ikipulizwa kwenye maeneo hayo tatizo linakwenda chini.

Akizungumzia zaidi kuhusu hali ya maambukizo ya ugonjwa wa malaria nchini Dkt Gwajima amesema jitihada zinazofanyika kutokomeza ugonjwa huo nchini zinafanikiwa kwani maambukizo ya malaria nchini yamepungua hadi asilimia 7.3 kutoka asilimia 14.8 mwaka 2015/16.

Amesema kupungua kwa maambukizi ya malaria kumetokana na kuwepo kwa mikakati mbalimbali ya kinga pia uwepo wa dawa zinazotumika kupambana na ugonjwa huo ambapo kiwango cha matumizi yake kilifikia asilimia 98.4, huku matumizi ya kipimo cha haraka cha kupima vijidudu vya malaria (mRDTs) ikifikia asilimia 97.8, lakini pia kumekuwa na ongezeko la matumizi ya vyandarua vyenye dawa kwa asilimia 62.5 mwaka 2017 kulinganisha na asilimia 55.9 mwaka 2015/16.

Kwa upande wake Meneja Mpango wa kudhibiti Malaria nchini Dkt Ali Mohamed amesema kulingana na takwimu za mwaka 2017, mikoa ya Kigoma, Kagera, Geita, Mara,Lindi, Ruvuma na Mtwara inaonekana kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya malaria.

Amesema kutokana na takwimu hizo, maeneo hayo yanayoonekana kuwa na kiasi kikubwa cha maambukizi ipo haja ya kupelekwa mikakati ya ziada mbali na mikakati ya kawaida ya kuzuia mbu, kuhakikisha kuna vitendanishi vya kupima malaria na dawa za kutosha zina ubora unaotakiwa.

Ameitaja mikakati ya ziada ni jinsi ya kutumia dawa kinga (SP) kwa ajili ya wanafunzi shuleni, pia kutoa dawa katika maeneo ambayo malaria inapatikana kwa kipindi kichache, na mikakati mingine ambayo hufanywa na Mpango wa kudhibiti Malaria nchini.

Juhudi za kuutokomeza ugonjwa wa malaria nchini, barani Afrika na duniani kwa ujumla bado una safari ndefu kwani kwa mujibu wa taarifa ya dunia ya malaria ya mwaka 2018 inaonyesha kuwa zimeripotiwa kesi milioni 219 za malaria duniani na kusababisha vifo 435,000.

Kadhalika barani Afrika, kati ya kesi zilizoripotiwa asilimia 70 zinatoka Afrika na idadi ya vifo asilimia 71 pia inatoka barani Afrika hasa katika nchi kumi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania. Nchi nyinginezo ni Burkina Faso, Cameroon, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ghana, Mali, Msumbiji, Niger, Nigeria na Uganda.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.