Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Utekelezaji Operesheni Anwani za Makazi wafikia asilimia 67

Imewekwa tar.: March 31st, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Innocent Bashungwa amesema kazi ya utekelezaji wa operesheni ya anwani za makazi kwenye mikoa yote Tanzania Bara imefikia asilimia 67 ya utekelezaji wake.

Waziri Bashungwa ameyasema hayo wakati wa kikao kazi kati ya Wakuu wa Mikoa, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia kuhusu uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa operesheni ya anwani za makazi nchini Jijini Dodoma hii leo.

“tumefikia asilimia 67 lakini bado tuna kazi kubwa ya kufanya, sina shaka na Wakuu wa Mikoa, naamini hili la operesheni ya Anwani za Makazi mtafanya vizuri” ,alisema Waziri Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa amesema kwa sasa kazi iliyobakia ni kuongeza hamasa kwenye kazi hiyo na kutoa elimu kwa wananchi ili kazi hiyo iendelee vizuri na kufikia malengo yanayotarajiwa na Serikali.

Naye Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nnape Nnauye amesema zoezi la utekelezaji wa operesheni ya anwani za makazi limekwenda vizuri na linatarajiwa kukamilika kabla ya muda uliopangwa ambao ni tarehe 22 Mei, 2022 ikiwa ni pamoja na kukamilisha Mfumo wenyewe wa anwani za makazi ambao upo chini ya wizara yake.

Waziri Nape Nnauye amesema kwa hivi sasa Serikali inaendelea kutambua maoni yaliyotolewa, kutoa elimu kwa wananchi, kuandaa taarifa, kutengeneza taarifa hizo na kuziingiza kwenye mfumo ikiwa ni pamoja kuuweka mfumo wenyewe ili ufanye kazi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe amesema lengo la kikao kazi ni kujadili namna ambavyo Wakuu wa Mikoa wanaendelea kutekeleza operesheni ya anwani za makazi Tanzania Bara lakini pia zoezi hili linaendelea na Zanzibar kazi ambayo inakwenda sambamba na Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika mwezi Agosti, 2022.

Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela amesema zoezi la anwani za makazi linaendelea vizuri kama ambavyo wizara iliwapa maelekezo kwani fedha za kazi hiyo zilipokelewa ijapokuwa kuna maeneo machache ambayo yalikuwa na tatizo la kimtandao wakati wa kutumia fedha za kazi hiyo.

Amesema baadhi ya changamoto zilijitokeza ni uwingi wa watu kwa baadhi ya mikoa pamoja na maeneo makubwa ya makazi lakini wanashukuru wizara zilituma timu za wataalam katika kusaidia utekelezaji wa kazi hiyo.

Zoezi la anwani za makazi linafanywa na wizara mbili kwa pamoja ambazo ni Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ambalo linatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 22 Mei mwaka huu kama ilivyoagizwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wakati akilizindua mnamo Februari, 8 mwaka huu.



Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.