Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

UMISSETA kufanyika Dodoma mwakani

Imewekwa tar.: June 9th, 2018

UMISSETA kufanyika Dodoma mwakani

Na Mathew Kwembe, Mwanza

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa ametangaza kuwa mashindano ya michezo ya Umoja wa Michezo wa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) na Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) yatafanyika mkoani Dodoma.

Kwa miaka mitatu mfululizo mashindano hayo yamekuwa yakifanyika mkoani Mwanza katika viwanja vya chuo cha ualimu Butimba.

Akifungua rasmi mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA kwa mwaka huu katika uwanja wa CCM Kirumba jana Waziri Mkuu alisema kuwa pamoja na mkoa wa Mwanza kufanya maandalizi mazuri ya kuwapokea wanafunzi zaidi ya 6000 wa shule za msingi na sekondari mashindano hayo hayana budi kufanyika katika mkoa mwingine.

Waziri Mkuu alisema kuwa serikali inatambua na kuthamini sana mchango wa kuwepo kwa mashindano hayo katika kuibua vipaji vya wanafunzi katika michezo mbalimbali, hivyo akawataka wadau wa michezo nchini kuunga mkono juhudi hizo ili vipaji vya wanafunzi hao viweze kuendelezwa.

Mhe.Majaliwa aliwaasa wanamichezo wanaoshiriki mashindano hayo kutambua fursa zilizo mbele yao kwani michezo ina nafasi kubwa katika kutoa ajira.

“Chezeni kwa malengo, natambua uwepo wa viongozi wa vilabu vya Simba, Azam na hata Yanga wapo hapa, naamini wakiridhika na vipaji vyenu watawachukua na kuwalea katika kambi zao” alieleza.

Hata hivyo Waziri Mkuu aliwaagiza walimu na Maafisa Elimu waliopo katika timu hizo kuhakikisha kuwa hawatowaruhusu wasio wanafunzi kushiriki michezo hiyo.

“Tukigundua kuwa kuna mkoa una timu yenye wanafunzi mamluki hatua kazi zitachukuliwa dhidi yao,” alionya Waziri Mkuu.

Pamoja na kuwataka waheshimiwa madiwani kutenga bajeti ya kutosha kuendeleza michezo katika halmashauri zao aliwahimiza walimu kuhakikisha kuwa wanafundisha somo la haiba ya michezo shuleni.

Aliwakumbusha walimu kutumia vipindi vya michezo kufundisha michezo huku akisisitiza kuwa walimu wenye taaluma ya michezo ndiyo wapangiwe kufundisha vipindi hivyo na siyo vinginevyo.

“Michezo ifundishwe na wenye taaluma ya michezo msipeleke waelekezaji kufundisha michezo hiyo shuleni,” alisema.

Aliongeza kuwa hata kwenye mashindano haya anatarajia kuona kuwa washiriki ni walimu wa michezo badala ya kuleta walimu wasindikizaji.

Alisema kuwa tayari Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli ameagiza kuwa michezo ichezwe tangu ngazi ya awali.

Kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzungumza, Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu Mhe. Joseph Kakunda alisema kuwa mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA yameliletea heshima kubwa taifa kwa kuibua vipaji vya wanamichezo mahiri.

Mhe.Kakunda aliwataja baadhi ya wanamichezo hao kuwa ni pamoja na Mbwana Samata, Edibily Lunyamila, Leodger Tenga na wengineo kwa umahiri wao mkubwa ambao chimbuko lake lilianzia katika mashindano haya.

Aliongeza kuwa mbali ya sekta ya michezo kuleta burudani katika taifa lakini imekuwa ni sekta muhimu kiuchumi huku akitolea mfano wa nchi ya Brazil ambayo kupitia sekta hiyo imeweza kuinua uchumi wake.

Pia Mhe.Kakunda alimuomba Waziri Mkuu kuhakikisha kuwa taifa linawekeza katika michezo kwa bajeti ya michezo kuboreshwa hasa katika ngazi za halmashauri.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Dkt Leonard Akwilapo ambaye alimwakilisha Waziri wake Profesa Joyce Ndalichako pamoja na kupongeza kuendelea kufanyika kwa michezo hiyo alisema kuwa wizara yake itaendelea kuboresha mitaala ya michecho mashuleni

Mapema Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bwana Tixon Nzunda alisema kuwa katika mashindano ya mwaka huu jumla ya wanamichezo 3,360 kutoka mikoa 28 ikiwemo miwili kutoka Zanzibar wanashiriki kwenye UMISSETA  ambapo michezo 10 itashindanishwa.


Kwa upande wa UMITASHUMTA alisema kuwa jumla ya wanamichezo 3120 kutoka mikoa 26 ya Tanzania bara watashiriki ikiwa ni wachezaji 120 kila mkoa.


Jumla ya michezo 9 ikiwemo mpira wa miguu wavulana na wasichana, mpira wa miguu maalum (wavulana viziwi), Netibali kwa wasichana, mpira wa wavu, mikono, kengele kwa wasioona, riadha maalum, riadha kawaida na sanaa za maonyesho.

Naye Naibu Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Juliana Shonza pamoja na kumshukuru Waziri Mkuu kwa nasaha zake alisema kuwa wizara yake kwa kuwa ndiyo yenye dhamana ya michezo itaendelea kuisimamia sera ya michezo nchini.





Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.