Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

Imewekwa tar.: January 20th, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani S. Jafo ameuagiza uongozi wa Jiji la Dodoma kufanya ukarabati wa Shule ya Msingi Nkuhungu iliyopo katika Jiji hilo ndani ya siku 14 ili kumaliza adha ya wanafunzi kusoma katika mazingira yasiyo rafiki kwao.

Waziri Jafo amefikia hatua hiyo hii leo tarehe 20 Februari, 2021 alipofanya ziara katika shule hiyo ambapo ilimlazimu kutoa maelekezo ya awali, alipovinjari darasa la awali na kukuta halina paa wala michoro ambayo ingeweza kuwasaidia Watoto kujifunza kwa weledi.

“Hili ni darasa la awali nilitegemea nikiingia humu, nione michoro ya aina mbalimbali ambayo inamsaidia Mwalimu anapofundisha na pia inakuwa rahisi kwa mtoto kujifunza kwa wepesi. Sasa naagiza darasa hili likarabatiwe kwa kupigwa plaster, na rangi lakini pia ichorwe michoro ya vitu mbali mbali” alisema Jafo.

Akiwa anaendelea na ziara yake katika shule hiyo, alilazimika kufanya kikao cha pamoja cha Walimu na Wanafunzi, ambapo alijitolea kuwa mlezi wa shule hiyo na kuutaka uongozi ufanye marekebisho kwenye vyumba 16 vilivyojengwa pamoja na darasa moja lililojengwa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Antony Mavunde.

“Lakini agizo langu mimi nataka  mkamilishe ukarabati wa shule hii, nawapa wiki mbili  mimi nitarudi hapa tena tarehe 20 Februari,2021, kwa ajili ya kuona ukarabati uliofanyika, maana hapa mkijipanga vizuri sio zaidi ya shilingi milioni 25 mtabadili kabisa mazingira ya kufundushia na kujifunzia Amesema Jafo.

Awali akisoma taarifa ya shule, Mkuu wa Shule ya Msingi Nkuhungu, Bernard Chanai, amesema kutokana na wingi wa wanafunzi katika shule yao, mpango uliopo sasa ni kujenga shule mpya mbili katika eneo la Ndachi ili kupunguza idadi ya wanafunzi na kufikia lengo la kisera la kuwa na wanafunzi 915 kwa shule.

Chanai amesema, Serikali ya awamu ya tano kupitia Halmashauri ya Jiji la Dodoma, walitoa shilingi milioni 545 ikiwa ni mpango wa ndani wa mwaka wa fedha, 2018/19 na 2020/21, fedha ambazo zinafanikisha ujenzi wa shule za Mnyakongo na Mtupe ambazo kila moja imeanza kwa kujengewa vyumba 10 vya madarasa, Matundu 9 ya vyoo sambamba na ujenzi wa jengo la Utawala, ikiwa ni mkakati wa Jiji kukabiliana na wingi wa wanafunzi.

Wakati huo huo Waziri Jafo ametembelea Shule ya Sekondari ya Itega, ambapo akiwa shuleni hapo alionekana kukerwa na hali ya matokeo mabovu ya kidato cha Nne kwa mwaka uliopita, kufuatia shule hiyo kutopata ufaulu wa daraja la kwanza mbali ya shule husika kuwa eneo la mjini.

“Hapa ni mjini miundombinu yote mnayo, mnashindwa vipi na shule nyingine zipo kijijini kabisa, suala hili halikubaliki, lazima muongeze bidii katika kufundisha” aliuambia uongozi wa Shule hiyo pamoja na Walimu.

Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa mbele ya Waziri Jafo, Ufaulu katika Shule ya Sekondari Itega, unaonesha ufaulu kwa mwaka ulipita, ulianzia daraja la pili ambapo ilikuwa ni wanafunzi 3, daraja la tatu wanafunzi 14, daraja la Nne, wanafunzi 62 na sifuri ilikuwa wanafunzi 25.

Akitoa Salamu za Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Benelith Mahenge, alisema mkoa umeendelea kujidhatiti katika suala la elimu kwa kila Wilaya na masuala mengine ya kiuchumi pamoja na suala la ulinzi na usalama.

Waziri Jafo, alikuwa katika ziara ya siku moja katika Wilaya ya Dodoma na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ujumla ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kikazi kote nchini.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nkuhungu, wakimsikiliza Waziri Jafo, alipo tembelea shule hiyo na kuzumza nao, hayupo pichani

Mhe. Waziri Jafo akiwa picha ya pamoja na wanafunzi wa shule hiyo.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.