Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yazishukia shule binafsi zinazolazimisha wanafunzi kurudia madarasa

Imewekwa tar.: January 28th, 2019

Serikali imewataka wazazi wenye watoto wanaosoma shule binafsi ambao watoto wao wamelazimishwa kurudia darasa kwa kigezo kuwa hawajafikia wastani wa ufaulu wa shule hizo wapeleke malalamiko yao kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ili yafanyiwe kazi kwani kitendo hicho ni kinyume na mwongozo uliotolewa na serikali.

Aidha alisema kuwa ili mtoto aweze kuruhusiwa kukariri darasa ni lazima mzazi aridhike na uamuzi huo kwani kitendo cha kuwalazimisha wazazi ni kinyume cha mwongozo na maagizo ya serikali.

Agizo hilo limetolewa jana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Mwita Waitara wakati akifungua mafunzo elekezi ya siku mbili kuhusu utekelezaji wa programu ya lipa kulingana na matokeo katika sekta ya elimu yanayofanyika jijini Dodoma.

Alisema kuwa hakuna sababu kwa mwanafunzi kulazimishwa kukariri darasa ikiwa alifaulu mitihani yake ya darasa la nne na kidato cha pili kwani mitihani hiyo ndiyo pekee inayoruhusiwa na serikali kupima uwezo wa mwanafunzi husika kuendelea na masomo ya juu.

“Nimekuwa napata malalamiko mengi kutoka kwa wazazi kuhusiana na jambo hili, na kama kuna mzazi anasema motto wake amelazimishwa kurudia darasa aende ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri  husika ili malalamiko yake yaweze kushughulikiwa,” alisema na kuongeza:

“Haiwezekani mtoto afaulu mtihani wa kidato cha pili, cha tatu, lakini pale tu anapofika kidato cha nne baadhi ya wamiliki wa shule huwalazimisha watoto hao kurudia darasa au huwataka wafanye mtihani wa kidato cha nne lakini wajiandikishe kama watahiniwa binafsi ndipo waruhusiwe kuendelea na masomo katika shule hizo,” alisisitiza Naibu Waziri.

Kwa mujibu wa Mhe.Wazitara, mtindo huu unaofanywa na baadhi ya wamiliki wa shule binafsi umekuwa ni kero kubwa kwa wazazi wenye watoto wanaokumbwa na kadhia hiyo kwani wazazi wamekuwa wakilazimika kulipa ada mara mbili ili watoto wao waweze kuruhusiwa kuendelea na masomo katika shule hizo.

Naibu Waziri aliongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi, na Teknolojia ilikwishatoa mwongozo kuhusu suala hilo na kwamba walimu wanaotakiwa kufundisha katika shule wanatakiwa wawe ni wale wenye sifa zinazostahili.

Pia aliwataka waajiri wa shule hizo kuhakikisha kuwa walimu wanaofundisha katika shule hizo wana mikataba ya ajira na pia makato yao ya kila mwezi yapelekwe kwenye mifuko ya jamii.

Jambo lingine alilolitolea ufafanuzi Naibu Waziri ni suala la Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanasimamia fedha za halmashauri ili zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Mhe.Waitara alionya kuwa ni marufuku kwa fedha za miradi ya elimu kutumiwa kufanya shughuli nyingine kinyume na maelekezo ya serikali.

“Kama Mkurugenzi unataka kubadilisha matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya elimu ni lazima uwasiliane na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa ajili ya kuomba idhini ya kufanya hivyo,” alisema.

Kuhusu kuhakikisha ubora wa elimu katika shule, Naibu Waziri alitaka Maafisa Elimu Kata kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao vizuri kwani bila watendaji hao kuwajibika ipasavyo katika kata zao, maendeleo ya elimu katika ngazi hizo yataendelea kuwa duni.

Aliongeza kuwa changamoto za elimu zipo za aina nyingi ambapo licha ya walimu kuwa na sifa za kufundisha lakini kama hawawajibiki ipasavyo maendeleo ya shule lazima yatakuwa chini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Elimu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Julius Nestory aliwataka watendaji hao wa elimu katika halmashauri kuhakikisha kuwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya elimu zinatumika kwa shughuli husika.

Aliongeza kuwa serikali hivi sasa haitamvumilia mtendaji yeyote yule wa halmashauri ambaye atatumia fedha za serikali kinyume na maelekezo na kutoa onyo kwa waweka hazina watakao wapotosha wakurugenzi wa halmashauri kuhusu jambo hilo.

Mafunzo hayo elekezi kuhusu utekelezaji wa program ya lipa kulingana na matokeo katika sekta ya elimu yanafanyika kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisaelimu wa Mikoa, Wadhibiti Wakuu Ubora wa Shule wa kanda, Maafisaelimu msingi na Sekondari, na Wadhibiti Wakuu Ubora wa Shule wa Wilaya kutoka halmashauri za mikoa ya Morogoro na Dodoma.

Programu ya Lipa kulingana na Matokeo ilizinduliwa mwezi septemba, 2014 chini ya mpango wa Matokeo Makubwa sasa kwa lengo la kuinua ubora wa elimu nchini. Kupitia program hiyo fedha hutolewa kwa kukidhi vigezo vilivyokubalika baada yua kufanyiwa  uhakiki na kuthibitika.

Tangu kuanza kutekezwa kwa program hii mwaka 2014/2015 Mamlaka za Serikali za Mitaa zilipokea  shilingi bilioni 15.53, na mwaka 2015/2016 jumla ya shilingi bilioni 22.36 na mwaka 2016/2017 jumla ya shilingi bilioni 40.09 zilipokelewa.

Anaandika  Mathew Kwembe


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.