• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Serikali kuajiri walimu 6000 mwaka huu

Imewekwa tar.: January 21st, 2019

Na Mathew Kwembe, Chemba, Dodoma

Serikali imesema kuwa mwaka huu inatarajia kuajiri walimu wapya 6000 wa masomo ya Sayansi na Hesabu ambapo tayari kibali cha kuwaajiri walimu hao kimekwishatolewa.

Aidha Serikali inakusudia kuwapeleka walimu 11,000 wa masomo ya sanaa ambao ni wa ziada waliokuwa wakifundisha shule za sekondari kufundisha shule za msingi ili kukabiliana na upungufu wa walimu unaozikabili shule za msingi nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia elimu Mhe.Mwita Waitara ameyasema hayo jana katika Wilaya Chemba, mkoani Dodoma wakati akizungumza na watumishi kutoka Idara za Elimu ya Msingi na Sekondari kutoka Halmashauri hiyo.

Kauli hiyo ya Serikali inafuatia taarifa ya Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Chemba bwana Josephat Ambilikile kumweleza Naibu Waziri kuwa Halmashauri ya Chemba ina upungufu wa walimu 808 kati ya walimu 1628 wanaotakiwa kufundisha katika shule za msingi 103 zilizopo katika wilaya hiyo.

Mhe.Waitara alisisitiza kuwa Serikali kuanzia mwaka huu itakuwa ikiajiri walimu kila mwaka ili kufidia walimu wanaostaafu na pia kukabiliana na upungufu unaotokana na ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule za msingi kutokana na mwitikio wa wazazi kupeleka watoto wao shule kufuatia uamuzi wa serikali ya awamu ya tano kutoa elimu ya bila malipo.

“Tayari Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli amekubali walimu waajiriwe na kibali kimekwishatolewa hivyo walimu 6000 wa masomo ya sayansi na hesabu na pia walimu 11,000 ambao ni walimu wa ziada waliokuwa wakifundisha masomo ya sanaa katika shule za sekondari watapelekwa kufundisha shule za msingi,” alisema Mhe.Waitara.

Pamoja na kueleza juhudi hizo za serikali za kuongeza idadi ya walimu, Naibu Waziri aliwataka walimu wanaofundisha masomo ya sayansi na hesabu kutowakatisha tamaa wanafunzi wanapowafundisha wanafunzi masomo hayo badala yake watumie mbinu rahisi ili wanafunzi waelewe kwa urahisi masomo hayo.

“Tunatarajia Walimu wanapaswa kutumia mbinu rahisi wanapofundisha hesabu ili wanafunzi wapende somo hilo,” alisema na kuongeza:

“Hata utunzi wa vitabu vya kufundishia masomo hayo inabidi uangaliwe upya kwani watoto wanakimbia kusoma masomo ya sayansi na hesabu kwani kutokana na namna vitabu hivyo vinavyotungwa vinasababisha watoto wachukie masomo ya sayansi na hesabu,” alisema Waitara.

Jambo lingine alilolizungumzia Naibu Waziri ni kiwango duni cha ufaulu kilichoonyeshwa na Mkoa wa Dodoma hasa wilaya ya Chemba katika matokeo ya kitaifa ya darasa la saba na kidato cha nne ambapo aliwataka watendaji wa elimu katika halmashauri hiyo kuja na mikakati itakayoboresha elimu wilayani humo.

“Ukitaja wilaya 10 zilizofanya vibaya kwa ufaulu Chemba ni ya 10 kwa matokeo ya darasa la saba, mkae chini mje na mkakati wa kuboresha matokeo ya wilaya yenu, cha muhimu mikakati hiyo ishirikishe ngazi zote kuanzia ngazi ya mkoa, wilaya, tarafa hadi kata,” alisema.

Pia Naibu Waziri alikemea tabia iliyojitokeza hivi karibuni kwa baadhi ya watendaji wa elimu kushiriki katika kuiba mitihani ambapo aliagiza kuwa kama kuna mwalimu ameshiriki katika wizi wa mitihani halmashauri isisite kumchukulia hatua kwani kitendo hicho kinarudisha nyuma maendeleo ya elimu ya nchi.

Sambamba na hilo Mhe.Waitara alionya tabia ya baadhi ya watendaji wasio waaminifu katika halmashauri kutumia kinyume na maelekezo ya serikali fedha za miradi kwa ajili ya kusaidia miundombinu ya shule.

“Fedha kama ni kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ipokee na iende ikajenge hosteli, kadhalika kama fedha ni kwa ajili ya kununulia samani za shule ipokee na iende ikanunue samani za shule, ukigusa fedha ya elimu kinyume na maelekezo ya serikali tutashughulika na wewe,” alionya Waitara.

Mapema Naibu Waziri alipata fursa ya kutembelea shule ya sekondari na shule ya msingi ya Chemba na kushuhudia ujenzi unaoendelea wa chumba kimoja cha darasa katika shule ya sekondari chemba, ujenzi ambao umetokana na michango ya wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mheshimiwa Simon Odunga alimweleza Naibu Waziri kuwa  wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na upungufu wa walimu na kukosekana kwa utayari kwa jamii kuchangia masuala ya elimu kwa dhana kuwa kila kitu kinatolewa bure na serikali.


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BODI YA MIKOPO YA SERIKALI ZA MITAA KUSUKWA UPYA

    January 23, 2023
  • MAKAMU WA RAIS AWAPONGEZA DODOMA JIJI KWA UWEKEZAJI

    January 20, 2023
  • SERIKALA YASISITIZA KILA MMOJA KUTUNZA MAZINGIRA

    January 20, 2023
  • TANZANIA ITAENDELEA KUSHIRIKANA NA WADAU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

    January 20, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.