Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Sera mpya ya ugatuaji wa Madaraka kuzipa nguvu ya kiuchumi Serikali za Mitaa

Imewekwa tar.: November 19th, 2018

Na Mathew Kwembe

Serikali imesema kuwa sera mpya ya ugatuaji wa madaraka kwa wananchi imezingatia katika kuzipa uwezo zaidi wa kiuchumi Mamlaka za Serikali za Mitaa ili ziweze kutekeleza ipasavyo majukumu yake ya kuwahudumia wananchi.

Sera hiyo ya Ugatuaji wa Madaraka inatarajiwa kuibadili sera ya sasa ambayo iliandaliwa takribani miaka 20 iliyopita, ambayo kutokana na mazingira ya sasa serikali imeona ipo haja ya kuibadili ili iendane na matarajio ya nchi ya kufikia maendeleo ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Akifungua kikao cha kujadili mapitio ya andiko la awali la sera ya Ugatuaji wa Madaraka (D by D) na taarifa ya mapitio ya mgawanyo wa majukumu kati ya Serikali Kuu, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa leo jijini Arusha, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bwana Tixon Nzunda amesema sera mpya ya ugatuaji madaraka itaziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwa na nguvu zaidi kiuchumi na hivyo zitaweza kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema kuwa ikiwa Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaweza kuandaa mazingira bora ya kibiashara na kusimamia viwanda katika maeneo yao ni wazi kuwa huduma kwa wananchi zitaboreshwa.

“Mamlaka za Serikali za Mitaa zikiwa na uwezo wa kiuchumi, zikawa na uwezo wa kuandaa mazingira bora ya biashara, zikawa na uwezo wa kuandaa viwanda katika ngazi ya maisha yao, vitakwenda kubadilisha mfumo wa kilimo chetu, zitakwenda kufanya mabadiliko ya mfumo wa utoaji huduma, lakini pia zitakwenda kuongeza uzalishaji katika Nyanja zote,” alisisitiza.

Naibu Katibu Mkuu aliongeza kuwa serikali inalenga katika kuongeza nguvu ya kiuchumi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuziwezesha Mamlaka hizo kukusanya mapato makubwa na hivyo kuzifanya kutokuwa tegemezi katika utoaji wa huduma muhimu kwa mfano huduma za elimu, utoaji wa huduma za afya na utoaji wa huduma za maji, makazi na huduma nyinginezo muhimu kwa jamii.

“Tunataka kuwa na Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa zenye nguvu ya kiuchumi ya kujiendesha zenyewe kiuchumi, kutoa huduma bora, lakini bila kusahau suala zima la utawala bora tukianzia kwenye suala zima la ushirikishwaji wa wananchi, kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa na sauti ya kuzisimamia serikali katika ngazi za vijiji, vitongoji lakini pia wananchi wanakuwa na uwezo wa kushiriki kupanga maendeleo yanayohusu maisha yao katika Nyanja zote za kiuchumi na kijamii,” alisema Naibu Katibu Mkuu.

Pia Bwana Nzunda aliongeza kuwa mapendekezo ya rasimu ya sera hiyo mpya imesisitiza kuwa katika utawala bora watumishi wanakuwa na weledi, waadilifu na wenye uwezo wa kuleta mabadiliko yanayotarajiwa na serikali kutokana na utekelezaji wa sera hiyo.

Mapema kabla ya kumkaribisha Naibu katibu Mkuu ili kufungua kikao hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Kisekta kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt Andrew Komba alisema kuwa kikao hicho kinalenga kujadili,na kuchakata mapitio ya rasimu ya sera mpya ya ugatuaji wa madaraka kwa umma.

Alisema kuwa mapitio ya sera mpya ya Ugatuaji wa Madaraka yanalenga kuboresha sera ya sasa ya Ugatuaji wa Madaraka ambayo ilitayarishwa mwaka 1998ili iweze kuendana na mazingira ya sasa ya utendaji kazi katika Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Dkt Komba aliongeza kuwa  Serikali inataka sera mpya ijikite katika kuwaandaa wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi.

Alisema kuwa Serikali za Mitaa ndani ya sera hii zinatazamiwa zisimamie mabadiliko ya kiuchumi jambo ambalo halikuwa likisimamiwa katika sera iliyopita.

“Mapendekezo ya rasimu ya sera hii yamezingatia katika kuhakikisha kuwa Serikali za Mitaa zinasimamia vizuri kilimo, Sera ya nchi ya viwanda ili kuendana na malengo ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa na viwanda ili kukuza uchumi, lakini vile vile ofisi ya Rais TAMISEMI mwaka jana ilikuja na tamko la kuwa na viwanda 100 kila mkoa,” alisema Dkt Komba na kuongeza kuwa:

“Tunataka Sekretarieti za Mikoa na  Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kusimamia uratibu wa uanzishwaji wa uchumi wa viwanda kwa kushirikisha sekta binafsi lakini vile vile kushirisha wadau wengine wa maendeleo”.

Kwa upande wake mmoja wa walioandaa rasimu ya andiko la sera hiyo Dkt Richard Mushi kutoka shirika lisilo la kiserikali la REPOA alisema kuwa katika siku za hivi karibuni Ofisi ya Rais TAMISEMI imejikuta ikishughulikia majukumu makubwa mfano afya  na elimu ambayo kimsingi hayamo katika sera ya sasa ya ugatuaji wa Madaraka lakini imeyaweka katika sera mpya ya ugatuaji.

Naye Mtaalamu wa Sera kutoka Shirika la Kimataifa la kuhudumia watoto UNICEF Dkt Pius Chaya alisema kuwa UNICEF kama Shirika la Umoja wa Mataifa iliamua kufadhili mradi huo baada ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kuona umuhimu wa kuhuisha sera ya ugatuaji ambayo iliandaliwa miaka 20 iliyopita.

Aliongeza kuwa UNICEF kama wadau wa maendeleo wana mchango mkubwa katika ushirikishwaji wa wananchi hasa katika ngazi ya chini kupitia Mamlaka zao za Serikali za Mitaa.

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.