Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

OR-TAMISEMI wafafanua utaratibu wa kuwapata wanafunzi wa bweni

Imewekwa tar.: January 4th, 2023

NA OR-TAMISEMI


SIKU za hivi karibu zimeibuka hoja ya wananchi wengi ambao wamehoji namna ya kuwachagua wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza kwa shule za bweni.

Hoja za wananchi zinaonesha wazi kuwa kila mzazi anatamani  mtoto wake achaguliwe katika shule za bweni.

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wazazi na walezu,

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- TAMISEMI anayesimamia Elimu, Dkt. Charles Msonde  amesema kuna vigezo wazi ambavyo vinatumika kuchagua wanafunzi hao.

Dkt. Msonde ametoa ufafanuzi huo mwishoni mwa wiki wakati wa ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ya  kukagua ujenzi wa miundombinu ya madarasa yatakayopokea wanafunzi wa kidato cha kwanza,2023.

Alisema kuwa wanafunzi waliofaulu na kuwa na sifa ya kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza  mwaka 2023 ni 1,073,941 na kati ya hao waliochaguliwa kujiunga na shule za bweni ni 4,224  ambao ni sawa na asilimia 0.39 ya wanafunzi wote waliochaguliwa.

Akifafanua ni kwa nini idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kwa shule za bweni ni ndogo, Dkt. Msonde alisema ni kutokana na ufinyu wa shule za bweni,

Alisema kuwa idadi ya shule za Sekondari za Serikali zinazochukua wanafunzi wa kidato cha kwanza ni 4,307 na kati ya hizo shule za kutwa ni 4,269 na za bweni ni 38 tu ambazo zinauwezo wa kuchukua wanafunzi 4,224.

"Kutokana na idadi ndogo ya shule za bweni tulizonazo na ili watoto waweze kukaa darasani vizuri, kulala bwenini kwa mujibu wa muongozo, shule hizo 38 zina uwezo wa kupokea wanafunzi 4,224 ambao ni sawa na asilinia 0.39 tu ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza."

Akizungumzia namna ya kuwapata wanafunzi kujiunga na shule za bweni, uchaguzi wa wanafunzi hao umekuwa ukizingatia vigezo mbalimbali ikiwemo ya kuzingatia viwango vya ufaulu.

"Wale wenye viwango vya juu sana ndio waliochaguliwa, lakini hata hivyo waliofaulu kwa viwango vya juu pia ni wengi, hivyo mfumo ulitumika kuchagua wale waliofauli zaidi ya wenzao."

“Hapa tunasema waliochaguliwa kwenda bweni wamepata daraja la kwanza A, lakini ukiangalia waliopata daraja hilo wapo wanafunzi 50,475, hivyo hata kwenye daraja hili la kwanza ipo kanuni iliyotumika ya kugawa nafasi za wanafunzi waliofaulu vizuri."

Alisema  kuwa, shule za bweni zimegawanyika katika makundi matatu ambayo ni  kundi la kwanza ni lile lenye ufaulu wa juu, kundi la pili ni shule za bweni za ufundi na kundi la tatu ni shule za bweni kawaida.

Dkt. Msonde alisema kwa upande wa shule zenye ufaulu wa juu ziko saba zikiwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 932 ambao ndio waliopangiwa.

Pia, shule za bweni za ufundi ziko tisa zikiwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 1,323 wakai shule za bweni za kawaida zimechukua wanafunzi 1,816 na bweni umiliki wa mkoa 153.

" Ikumbukwe kuwa shule hizi za bweni ni za Kitaifa, hivyo uchaguzi wa wanafunzi wa kwenda katika shule hizo pia unafanyika kitaifa kwa maana kuwa kila mkoa na halmashauri nchini lazima zitoe wanafunzi watakaokwenda kusoma katika shule hizo."

"Hapa tunaona wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja kwanza (A) wako 50,475 na kati ya hao waliochaguliwa ni 4,224, hivyo kwenye shule za bweni zenye ufaulu wa juu tunatumia uwiano wa idadi wa watahiniwa katika mkoa  mara Idadi ya nafasi zote kwa watahiniwa waliofaulu zaidi gawanya kwa jumla ya watahiniwa wote kitaifa hapo utapata  idadi ya nafasi za bweni kwa watahiniwa waliofaulu zaidi kwenye Mkoa."

Dkt. Msonde aliongeza, "kanuni hiyo hiyo itatumika kwenye mkoa kupata idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kwenda kwenye shule zenye ufaulu wa juu kutoka mkoa husika."

"Kanuni hii pia itatumika kupata wanafunzi waliochaguliwa kwenye shule za bweni za ufundi kutoka kwenye mikoa yote nchini."

Kwa upande wa shule za bweni kawaida, Dkt. Msonde alisema kanuni yake ni uwiano wa watahiniwa wote wa Darasa la Saba katika shule za vijijini au mazingira magumu katika Halmashauri mara idadi ya nafasi zote za bweni kwa wavulana na wasichana wa vijijini au mazingira magumu Tanzania bara gawanya na idadi ya watahiniwa wote wa darasa la VII katika shule za vijijini/mazingira magumu hapo utapata nafasi kwa kila Halmashauri.

"Ikumbukwe kuwa nafasi hizi ni kwa wanafunzi wote waliosoma shule za Serikali na Binafsi katika Mkoa na Halmashauri husika."

Dkt Msonde alisema kwa shule za kutwa wanafunzi  1,069,717  walichaguliwa kwenda kwenye shule hizo ambapo kila wanafunzi aliyefaulu na kukosa nafasi kwenye ushindani wa shule za Bweni alipangiwa kwenye shule ya sekondari ya kutwa  iliyokaribu na shule ya msingi aliyosomea.

"Sambamba na kanuni na muongozo wa uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha kwanza mfumo ndio uliotumika kufanya chaguzi hizo hii kupunguza changamoto za kibanaadamu ambazo zingeweza kuleta mgongano wa kimaslahi."

Dkt. Msonde aliongeza kuwa: "kila mwanafunzi aliyechaguliwa kwenda shule ya bweni anakidhi vigezo vyote hata ukiingia kwenye mfumo utaona kuwa vigezo vyake ni vya juu kuliko wengine waliokwenda kwenye shule za kutwa katika hili  watoto wa Taifa hili kutoka pembe zote za nchi wenye vigezo wamechaguliwa kwenda kwenye shule za bweni ili kuleta utaifa na umoja kwa watoto wetu.

Alisema daraja la  A analipoata mwanafunzi ni kati ya jumla ya alama 241 hadi 300.

"Niweke wazi kuwa ufaulu wa daraja la kwanza yaani A unaanzia kwenye maksi 241 hadi 300,, na wazazi au walezi wanaona daraja ambalo mtoto wake amepata lakini sisi tunaoingia kwenye mfumo tunaona alama  sasa mtaona kwamba takribani wanafunzi  46,251 wenye ufaulu wa daraja la kwanza (A) wamepangiwa kwenye shule za kutwa kutokana na uhaba wa nafasi za bweni.

"Lakini wale waliopangiwa bweni wanaufaulu wa daraja la kwanza wa alama za juu zaidi kuliko wale 46,251 na ndio maana tulivyofika ukomo wa idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kwenda bweni wale waliobakia wenye ufaulu wa daraja la kwanza wote waliopangiwa kwenye shule za kutwa."

Aidha, Dkt. Msonde alitumia fursa hiyo kuwasihi wazazi kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza, 2023 wanaripoti shule kwa wakati ili waweze kuanza masomo kwa awamu moja.


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.