Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Naibu Waziri ataka wadau waje na mpango wa kuendeleza michezo

Imewekwa tar.: March 29th, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma,

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.George Waitara amewataka wadau na wataalamu wa michezo nchini kuja na mpango mahsusi wa namna nchi itakavyoweza kufikia  katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.

Akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kwa ajili ya Mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) na Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) kilichoandaliwa na kampuni ya vinywaji ya Coca cola, Mheshimiwa Waitara amesema anatamani kuona walimu na wadau wengine waje na mpango mahsusi wa kuendeleza michezo ili Tanzania iondokane na tabia ya kuwa kichwa cha mwendawazimu katika sekta hiyo.

Mhe.Waitara amesema wataalamu waje na hoja ya kuendeleza sekta na michezo na anaamini kuwa walimu katika hili wana mchango mkubwa katika kuendeleza sekta ya michezo.

Amesema kwa kuwa watanzania wanapenda sana michezo, hakuna sababu ya kuwasononesha na badala yake akataka wataalam wa michezo kuja na mpango kabambe wa kukwamua sekta hiyo.

Mhe.waitara amesema pamoja na mchango mkubwa unaofanywa na walimu nchini katika kuinua maendeleo ya elimu nchini ambapo kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kiwango cha ufaulu kimekuwa kikiongezeka, bado anaamini walimu wana jukumu kubwa katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanafundishwa michezo kwa nadharia na vitendo.

“ Natoa maelekezo kwa walimu wote kuhakikisha kuwa somo la michezo linafundishwa kwa nadharia na vitendo kama mtaala wa elimu unavyoelekeza,” amesema na kuongeza:

“ viwanja vya michezo vifufuliwe na vifanye kazi kama ilivyokusudiwa, viwanja vilivyovamiwa vipimwe na kuwekewa mipaka,” amesema.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya michezo ya umiseta na udhamini kutoka kampuni ya Coca cola, Naibu Waziri ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kudhamini mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika kitaifa mkoani Mtwara kuanzia mwezi juni mwaka huu.

Pia Mhe.Waitara ameipongeza coca cola kwa kuanzisha shindano maalum la kutafuta shule bora zinazoongoza kwa kutunza na kuhifadhi mazingira ambapo mtoto ambaye atafanikiwa kuokota chupa kilo 600 na kuendelea watapata zawadi mbalimbali zikiwemo laptop.

Naibu Waziri amewataka Coca cola kuhakikisha kuwa shindano hilo linazifikia shule nyingi iwezekanavyo na ikibidi lifanyike kwa mikoa yote 26 nchini.

Mhe.Waitara amewaagiza Maafisa Elimu wa Mikoa, na Maafisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazotolewa na kampuni hiyo zinagawiwa kwa walimu watakaoshinda na wanafunzi pia.

Wakati huo huo Naibu Waziri Waitara amewataka Maafisa elimu nchini kuhakikisha kuwa wanawasimamia walimu na wanafunzi ili waweze kupanda miti ya kutosha nchini ili waweze kukabiliana na athari za jangwa.

“Tukitaka kusaidia kampeni ya usafi wa mazingira hatuna budi kuanza na walimu na wanafunzi, tuhakikishe kila mwalimu shuleni anapanda mti mmoja na kila mwanafunzi anapanda miti miwili mmoja nyumbani na mwingine shuleni,” amesema.

Mapema Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Julius Nestory ameipongeza kampuni ya vinywaji ya Coca cola kwa kuendelea kudhamini mashindano ya UMISSETA ambapo mwaka huu kampuni hiyo imeongeza kipengele cha usafi wa mazingira.

Amewataka maafisa elimu kuhakikisha kuwa zawadi zote zitakazonunuliwa na wadhamini coca cola zinawafikia walengwa na kwamba zawadi na jezi hizo kamwe zisiishie mitaani kwa wasiohusika.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.