Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

MSIWE SEHEMU YA MIGOGORO MIONGONI MWENU NA JAMII ZENU - NZOWA

Imewekwa tar.: August 11th, 2024

Na Fred Kibano, Kilimanjaro

Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Kiseo Yusuf Nzowa amefungua mafunzo kwa Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata wa mkoa huo na kuwataka waondoe changamoto zao kwa kutokuwa sehemu ya migogoro kwenye maeneo yao. 

Bw. Kiseo Yusuf Nzowa ametoa kauli hiyo mapema leo tarehe 11 Agosti, 2024 katika ukumbi wa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata wa mkoa huo na kuwataka kuondoa changamoto zilizopo kwenye maeneo yao hususani migongano yao ya kiutendaji na migongano na jamii kwenye maeneo yao.

“nizitaje baadhi ya changamoto ambazo zipo, moja ni migogoro ya kiutendaji baina ya wataalam na Viongozi, au na wanasiasa katika maeneo yenu, unaweza ukakuta Mtendaji wa Kata haelewani na Afisa Tarafa wake, haelewani na mtu fulani, sasa hili ni tatizo kwa sababu huwezi kufanya kazi vizuri yenye mafanikio kwenye sehemu ambayo inachangamoto” alisema Bw. Kiseo Nzowa.

Aidha, Bw. Nzowa amewataka washiriki hao kuwa wabunifu na wadadisi ili kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwenye maeneo yao kwani Serikali bado inauhitaji mkubwa wa mapato kwa ajili ya kuhudumia wananchi ikiwemo miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa ambayo inahitaji fedha nyingi za Serikali ili ikamilike na kusisitiza kwamba ukusanyaji wa mapato ya Serikali ni roho na uti wa mgongo wa Tanzania. 

Bw. Ibrahim Minja ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha utendaji kazi kwa washiriki hao kwa kuzingatia majukumu yao na mpaka sasa mafunzo hayo yapo katika awamu ya tano na jumla ya mikoa 24 imekwishafikiwa na mafunzo hayo ambapo imebaki mikoa miwili ya Tanga na Iringa.

Naye Bw. Hussein Ally Kadangu Afisa Mtendaji Kata ya Bombo Halmashauri ya Wilaya ya Same mkoa wa Kilimanjaro ameishukuru Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kupeleka mafunzo hayo mkoani Kilimanjaro na kuahidi kwa niaba ya washiriki wenzake kwenda kuyatekeleza yale yote ambayo watafundishwa katika siku mbili za mafunzo kwenye maeneo yao. 

Mafunzo kwa Watendaji wa Kata na Maafisa Tarafa nchini yanatolewa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kupitia Programu ya Uimarishaji wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Regions and Local Government Strengthening Programme-RLGSP) kwa kushirikiana na Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo pamoja na Chuo cha Utumishi wa Umma na mpaka sasa jumla ya mikoa 24 imepata mafunzo.


Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • SANAA ZA MICHEZO ZINAPEWA KIPAUMBELE KATIKA UMITASHUMTA & UMISSETA 

    June 02, 2025
  • UMITASHUMTA & UMISSETA 2025 KUFANYIKA KITAIFA MKOANI IRINGA.

    May 31, 2025
  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.