Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Miradi ya TSCP yachochea uchumi Jiji la Mbeya

Imewekwa tar.: May 10th, 2019

Zaidi ya shilingi bilioni 14 zatumika katika ujenzi wa miundombinu ya barabara  na utengenezaji wa mitaro ya maji ya mvua katika Jiji la Mbeya jambo ambalo limesababisha uboreshaji wa mazingira na kuchochea uchumi wa Jiji  hilo.

Hayo yamesemwa na  Mhandisi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya na Mratibu wa Mradi wa Uimarishaji Miji (TSCP) Bw. Osward Kasambala wakati akitoa maelezo juu ya maendeleo ya Mradi huo kwa timu ya ufuatiliaji kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) iliyotembelea jiji hilo kwa lengo la kukagua maendeleo ya miradi iliyo chini ya  mradi wa uimarishaji Miji  Tanzania(TSCP)

Bw. Kasambala amesema Mradi wa Uimarishaji Miji Tanzania umesaidia ujenzi wa Miundombinu katika Jiji la Mbeya kwa kuboresha mazingira, kuongeza kasi ya uchumi, kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuongeza Mapato ya Halmashauri ya Jiji hilo.

“Awali miundombinu ya Barabara katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya ilikuwa ni vumbi lakini kwa sasa baada ya Mradi wa TSCP kujenga miundombinu hali imekuwa tofauti kwani miundombinu imebadilika na kuwa kivutio kwa wananchi kukuza uchumi wa Jiji la Mbeya” Anafafanua Kasambala

Amesema mara baada ujenzi wa miundombinu ya barabara Halmashauri ya Jiji la Mbeya imeweza kuchochea hali ya uchumi na kuweza kuongeza mapato kutokana na wananchi wengi kuwekeza kwenye maeneo ambayo barabara zimejengwa ukilinganisha na awali ambapo barabara nyingi zilikuwa za vumbi.

Bw. Kasambala amezitaja barabara zilizojengwa chini ya Mradi wa Uimarishaji Mji (Tanzania Strategic Cities – TSCP) katika kipindi cha mwaka 2018/2019  kuwa ni barabara ya MUST yenye urefu wa kilometa 2.7,  barabara  kutoka Ilomba hadi Ivumwe yenye urefu wa kilometa 1.8 na ujenzi wa  Mtaro wa maji ya mvua  wenye urefu wa kilometa 2.8.

Wakati huohuo Bi Debora Mkemwa kutoka Ofisi ya Rais Tawala zaMikoa na Serikali za Mitaa ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa usimamizi wa ujenzi wa miundombinu hiyo na kuwataka kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo kwa wakati na kuzingatia ubora na dhamani ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya mradi huo

Aidha  Jiji la Mbeya ni miongoni mwa majiji 5 na Halmashauri 3 ambazo zinanufaika na Mradi wa  uimarishaji wa miji unaosimamiwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na kufadhiliwa na Benki ya Dunia.

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI MBEYA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Fursa kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne 2024 kubadili Tahasusi na Kozi April 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA ZA AFYA - TAMISEMI 2025 March 15, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 23, 2025
  • PJT-MMMAM Yawezesha Uanzishwaji wa Vituo 206 vya Malezi ya Watoto Wadogo

    May 21, 2025
  • SERIKALI KUJENGA DARAJA LINALOUNGANISHA KIJIJI CHA NEGERO – KILINDI

    May 21, 2025
  • MHE. MCHENGERWA ABORESHA TAARIFA ZAKE KWENYE  DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.