Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Serikali yaanza kuandaa Mpango rasmi wa kukabiliana na uhaba wa watumishi

Imewekwa tar.: February 1st, 2022

Na Fred Kibano, Morogoro

Serikali imesema mafunzo juu ya orodha na maelezo ya kazi yatawezesha Mpango wa Serikali wa kupunguza uhaba wa watumishi Serikalini ambao unatokana na kutobainishwa kisayansi bila ya kuangalia uzito wa majukumu ya watumishi kwenye Taasisi za Serikali.

Akifunguzi mafunzo hayo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI mjini Morogoro hivi leo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Laurean Ndumbaro amesema uhaba wa watumishi Serikalini kwa sehemu kubwa unatokana na kutobainishwa kisayansi bila ya kuangalia uzito wa majukumu ya watumishi katika Tasisi za Serikali na ndiyo maana Mifumo ya kiutawala imekuwa ikiandaliwa na kutumika kukabiliana na uhaba huo.

Dkt. Ndumbaro amesema kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikiweka Mifumo mbalimbali ya kimenejimenti ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji kazi wa kila siku na hivyo zoezi hilo la kuandaa orodha ya kazi kwa wakati huu ni muhimu kwa kila Taasisi ya Serikali.

“Orodha ya kazi ni Mfumo wa Kimenejimenti unaowezesha kuainisha mahitaji kwa idadi na aina ya watumishi, cheo na majukumu yote yanayopaswa kutekelezwa kwa kila mtumishi katika kila cheo kwa mujibu wa muundo na mgawanyo wa majukumu ya Ofisi” alisema Dkt. Ndumbaro.

Aidha, amesema lengo sio kuwapunguza watumishi wa Umma bali ni kuangalia uhaba na upungufu mkubwa wa watumishi kwenye kada mbalimbali na kuweza kupunguza upungufu uliopo kabla ya kuajiri watumishi wengine ili kuboresha utendaji kazi wa shughuli za Serikali katika ngazi zote.

“hii itasaidia kubaini maeneo ambayo yanaupungufu mkubwa wa watumishi kuwa ni kiasi fulani na utoshelevu ni kiasi fulani ili tuweze kuwaondoa wengine kwenye maeneo ambayo wamezidi na kuwapeleka kwenye maeneo ambayo yanakabiliwa na upungufu mkubwa kabla ya kuajiri watumishi wapya” alisema Dkt. Ndumbaro.

Akitoa maelezo ya awali kwa niaba ya katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Prof. Rizikiki Shemdoe kabla ya hotuba ya mgeni rasmi, Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Mariam Ntunguja amesema mafunzo hayo yataleta tija kuanzia Ofisi ya Rais TAMISEMI Makao Makuu, Mikoa, Halmashauri na Tasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI.

“baada ya kukamilika kwa mafunzo haya kazi inayofuata ni kuandaa mahitaji ya watumishi kwenye ngazi ya Wizara, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi zilizopo chini ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa” alisema Ntunguja.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Rasilimali Watu Bwana Marko Masaya amesema Ofisi ya Rais TAMISEMI inaundwa na vitengo 6 na idara 11 ambapo idadi ya watumishi waliopo makao makuu ni 520 lakini pia kikosi kazi hicho kinawajumbe wapatao 32 hivyo zoezi la kuandaa orodha ya kazi na maelezo yake itasaidia kujua idadi ya watumishi kwa kuzingatia mahitaji halisi ya watumishi kwa kuzingatia muundo wa wizara.

Mwenyekiti wa kikao kazi hicho Bwana Boniface Luhende akiongea kwa niaba ya wajumbe wenzake amesema tangu mafunzo hayo yalipoanza yamekuwa na mafanikio na kwamba wataendelea kupokea maelekezo mbalimbali na kuyafanyia kazi ili kufanikisha azma ya kikao kazi hicho.



Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.