Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

JAFO: Wataalam fanyeni upya tathmini ya gharama za ujenzi Hospitali ya Uhuru.

Imewekwa tar.: September 13th, 2019

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amewataka wataalam wa ujenzi kutoka SUMA JKT na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kukaa chini na kutafakari namna ya kujenga hospitali ya Uhuru kwa gharama nafuu kulingana na fedha iliyopo sh bil 3.

Mhe Jafo ametoa maagizo hayo wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa hospitali hiyo na kupokea taarifa kutoka kwa msanifu majengo kutoka Suma JKT Bw. Michael Gama wanaojenga hospitali hiyo na kusema gharama za ujenzi ni sh bil 6.1.

Amefafanua kuwa hospitali hiyo inajengwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Magufuli kutokana na mapenzi yake kwa wananchi hivyo kushindwa kuikamilisha ina maanisha watu na vyombo vya serikali vimeshindwa kuendeleza juhudi zake.

“Mimi niwaagize wataalam kakaeni chini mtafakari jinsi gani tutajenga hii hospitali itajengwa lakini kwa style hii haiwezekani, angalau tungekuwa hatuna fedha lakini fedha tunayo bil 3, hivyo tafakarini nini kifanyike jengo hili liweze kujengwa” Amesisitiza Mhe. Jafo.

Ameendelea kusema,  litakuwa jambo la ajabu kama Nyang,wale na Kyerwa walipata sh bil 1.5 ujenzi wa hospitali na zimekamilika halafu hapa ishindikane kwa sh bil 3 na wataalam wote wapo hapa jambo hilo haliwezekani.

“Na ndio maana nilitaka majengo haya yapewe vyombo vya serikali maana wao ndio wanajua maono na dhamira ya Rais wetu katika kuhakikisha inakuwepo hospitali ya Uhuru,sasa mimi nimejivua kama waziri wake kazi yangu nataka jengo hili likamilike kwa gharama ya shilingi bilioni 3.

Ameendelea kuhoji kuwa kazi imeanza lakini shida ni kwenye gharama za ujenzi hivyo ujenzi utaanza lakini hautakamilika wakati dhamira ya serikali ni wananchi wapate huduma bora za afya, natamani tungeweka majengo yetu ya kawaida lakini kwa hapa ni tofauti hivyo sina uhakika wa kukamilisha ujenzi wa Hospitali hiyo.

 Wakati huohuo msanifu majengo kutoka SUMA JKT wamekubali kukaa chini  na kuangalia gharama za ujenzi katika usanifu ili kufikia muafaka wa kuendelea na ujenzi hadi kukamilika kwa gharama iliyotolewa na Serikali.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi huo  Bw. Gama amesema ujenzi wa mradi huo ulianza agosti 16 na kwa sasa wamefikia hatua ya uchimbaji wa msingi na matarajio yakiwa kukamilisha uchimbaji huo septemba 16 mwaka huu.

Hata hivyo amesema bado hawajasaini mkataba bali wamesaini makubaliano ya awali na ndio hayo wanayotumia kufanyia kazi kwa kuwa wanaendelea na mapatano ya gharama ya ujenzi.

Kwa upande wake mhandisi kutoka Wakala wa Majengo (TBA) Bw. Elias Tillya amesema ili kuendana na kiasi cha fedha kilichopo inabidi kupunguza mita za mraba za jengo ambazo ni 4400 kwa sasa.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Bw.  Athuman Masasi amesema hawakuridhishwa na gharama ya ujenzi ya shilingi bil 6 hivyo tayari walishafanya mazungumzo  na wataalam kuona haja ya kukaa pamoja na kuliona hilo.

“kwa mujibu wa utaratibu wa kisheria waliouweka ilikuwa tufanye negosition kati ya halmashauri na wao,sasa tulichoshauriana tukasema hebu fedha tulizotoa mil 900 kazi ifanyike ili tuone itaishia wapi wakati maelewano ya bei inaendelea,na ndio maana hatujafunga nao mkataba” Amesisitiza Bw. Masasi.

Aidha hospitali hiyo inajengwa baada ya Rais Magufuli kufuta sherehe za Uhuru mwaka jana na fedha zake kiasi cha sh bil 1.5 kuelekezwa kwenye ujenzi huo na kuongeza sh bil 1.5 nyingine zilizotokana na gawio la kampuni ya simu ya Airtel.

Na. Angela Msimbira CHAMWINO

Matangazo

  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert (extension) 1 May 28, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert (extension) May 28, 2025
  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

    May 30, 2025
  • Wamiliki wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana watakiwa kuzingatia miongozo na kanuni zilizopo.

    May 29, 2025
  • Mhe. Katimba awapokea Wabunge wa Zambia waliokuja kujifunza kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania Bara

    May 28, 2025
  • Mtwale Atoa Mwongozo kwa Makatibu Tawala Wasaidizi wa Mikoa

    May 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.