Swahili
  • English
  • Swahili
    • Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Machapisho
      • Taarifa za Mapato
      • Majarida
      • Fomu Mbali mbali
      • Presentations
      • Ramani za mradi wa BOOST
      • Program ya SCALE
    • Miongozo
      • Miongozo OR TAMISEMI
      • Miongozo ya Elimu
      • Green and Smart Cities
      • Miongozo ya Kilimo
      • Miongozo ya Afya
    • Michoro ya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
  • Maktaba ya Video

Jafo Aagiza Ianzishwe ‘One Stop Center’ kwa ajili ya Wawekezaji

Imewekwa tar.: June 12th, 2018

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewataka Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya nchini kuhakikisha wanaanzisha kituo kimoja cha huduma ‘One Stop Center’ kwa ajili ya wawekezaji.

Mhe. Jafo ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Warsha ya namna ya Uendeshaji wa  Mabaraza ya Biashara kwa Mikoa na Halmashauri zote Nchini iliyoandaliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Mradi wa Local Investiment Climate (LIC) inayofanyika kwa siku mbili Jijini Dodoma.

Katika Warsha hiyo inayowajumuisha viongozi wa Ngazi za Mkoa na Wilaya Mhe. Jafo amesema mazingira magumu ya upatikanaji wa taarifa za uwekezaji na urasimu uliopo katika Mikoa na Wilaya ndio unaowakwaza Wawekezaji katika harakati zao za kutaka kuwekeza katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

“Imekuwa ni vigumu sana kwa Muwekezaji kupata taarifa sahihi na kwa wakati katika maeneo yetu na hii imekua ikiwakatisha moyo na kupelekea hata kusitisha mpango mzima na nia yao ya kuwekeza katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, inatakiwa tubadilike na tuweke mazingira rahisi yatakayomuweza kila mdau anayetaka kuwekez kupata taarifa anazozihitaji kwa urahisi.

Hali hii inarudisha nyuma juhudi zetu za kuhamasisha uwekezaji sasa basi kila kiongozi wa Mkoa na Wilaya kuhakikisha wanaanzisha kituo kimoja “One Stop Center” ambacho kitatoa huduma zote kwa Wawekezaji kama vile upatikanaji wa maeneo ya uwekezaji, Leseni za biashara, Hati miliki, usajili wa kampuni, namna ya ulipaji wa kodi nk” alisema Jafo.

Aliongeza kuwa warsha hii imewakutanisha wadau kutoka Sekta ya umma na binafsi katika kila ngazi ya utawala ili kujadiliana namna bora ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji Nchini na hivyo basi ni wakati wa kukubaliana kwa pamoja namna mabaraza ya Biashara yatakavyosaidia katika kukuza Uchumi wa Viwanda ambao ndio muelekeo wetu kama Taifa kwa hivi sasa.

Sambamba na hilo Jafo aliwakumbusha viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwa pamoja na majukumu mengine wanapaswa kutengeneza mazingira bora ya kufanyia biashara na uwekezaji, kuibua fursa za uwekezaji, kuzinadi fursa zilizoibuliwa kupitia Makongamano ya uwekezaji na kuandaa midahalo mahususi.

Pia Mhe. Jafo alisisitiza kuwa mara baada ya kikao hiki kila kiongozi akahakikishe kuwa Vikao vya mabaraza ya Biashara vinafanyika kwa mujibu wa Sheria na viongozi washiriki katika vikao hivyo na maazimio ya vikao hivyo yakashughulikiwe kwa wakati na kutoa mrejesho kwa upande wa sekta za umma na binafsi.

Aidha kila Halmashauri zikatenge bajeti kwa ajili ya uendeshaji wa Mabaraza ya biashara  na kwa upande wa Sekta binafsia ziandae utaratibu mzuri wa kuchangia gharama za uendeshaji wa vikao hivyo.

Alimalizia kuwa Mradi wa LIC kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Baraza la Taifa la Biashara kuandaa utaratibu wa kueneza uzoefu uliopatikana katika Mikoa miwli ya Dodoma na Kigoma ambapo mradi huu umetekelezwa ili mikoa mingine iweze kujifunza na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.

Mabaraza ya Biashara Tanzania yameanzishwa kwa mujibu wa Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2001 na kuchapishwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 691 la tarehe 28 Seot,2001.

Matangazo

  • TOR - Msimbazi Watershed Management – Modelling May 26, 2025
  • Monitoring & Support, TOR - DMDP 2 SWM Service Framework & Delivery System in Dar May 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUJITOLEA KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA KADA YA ELIMU CHINI YA MRADI WA GPE - TSP May 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA YA MKATABA KWA KADA YA AFISA LISHE May 13, 2025
  • DMDP 2 Dar SWM Service Framework & Delivery System - REOI Advert May 12, 2025
  • Msimbazi Watershed Management - REOI Advert May 12, 2025
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Nipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kufikia malengo ya Mhe. Rais – Prof. Tumaini Nagu

    May 26, 2025
  • TARURA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    May 26, 2025
  • MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO 

    May 26, 2025
  • MAHUSIANO MAZURI  NI NGUZO MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU-MHE.SAGINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.