• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Dkt. Gwajima: Shirikisheni mipango yenu kwa viongozi wa serikali ngazi ya msingi

Imewekwa tar.: September 4th, 2019

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Dorothy Gwajima amewaagiza watumishi wa Sekta ya afya  ngazi ya  Msingi kuhakikisha wanashirikisha Viongozi wa Mitaa, Vijiji na Kata mipango yote ya afya inayohitaji ushirikishwaji wa wananchi.

Dkt. Gwajima ameyasema hayo leo wakati alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea vituo vya kutolea huduma kwa lengo la kujionea maendeleo ya utoaji wa huduma za afya kwa jamii pamoja na matayarisho ya vituo hivyo katika kushiriki huduma za afya ya kinga katika kijiji cha Mkoyo, Kata ya Hombolo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Amewataka watumishi hao  kuhakikisha wanawashirikisha viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali ili, somo la afya liweze kuwafikia wananchi wa makundi yote kokote waliko  kwa kuwa  ushirikiano huo ni muhimu katika kujenga uelewa na kufanyakazi kwa pamoja.

Dkt. Gwajima amefafanua kuwa, watumishi wa sekta ya afya ngazi ya msingi wanatakiwa kuwasiliana na Viongozi wa ngazi zote kuanzia Kitongoji, Mtaa, Kijiji, Kata hadi ngazi ya juu katika Halmashauri na Mkoa kuhusu masuala yote ya afya yanayohitaji ushiriki wa wananchi ili kuwezesha viongozi hawa kuibeba vizuri ajenda ya afya na kuwaelewesha wananchi.

Amewahimiza watumishi wa sekta ya afya ngazi ya msingi kuhakikisha nao wanagonga milango ya viongozi hawa na kuwapa ajenda za afya zinazohitaji ushiriki wa wananchi kwa kuwa viongozi hao ndiyo wenye dhamana ya kwanza kabisa ya uongozi wa wananchi hivyo, ni fursa kubwa endapo tutaendelea kushirikiana nao kwa karibu zaidi.

“kufanya kazi pamoja na viongozi wa serikali katika ngazi ya kitongoji, mtaa, kijiji, kata na ngazi zingine zote za uongozi wa serikali na jamii kutasaidia kuharakisha uelewa wa wananchi juu ya ajenda za afya na juhudi za serikali na hatimaye, kuwezesha wananchi wengi zaidi kushiriki shughuli za kijamii zinazolenga kuboresha afya ya jamii kwa ujumla ili, kujenga taifa lenye afya bora kwa gharama nafuu kabisa maana kinga ni bora kuliko tiba” Amesema Dkt. Gwajima

Amesema kuwa, viongozi wa ngazi ya kitongoji, mtaa, kijiji, kata na ngazi zingine zote wakielewa vizuri sera, miongozo na mipango mbalimbali ya serikali kuhusu afya ya jamii wataendelea kuwa mabalozi na wasimamizi wazuri wa kufikisha ujumbe kwa jamii kwa haraka na kuwezesha kuhamasisha jamii husika kushiriki katika masuala ya afya yanayohitaji wananchi.

Dkt. Gwajima amewashukuru viongozi mbalimbali wa serikali na jamii ngazi zote kwa ushirikiano wao wakati wote katika kuibeba ajenda ya afya na kufanikisha mambo mengi ikiwemo ujenzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za afya unaoendelea nchi nzima na masuala yote ya elimu ya afya kwa jamii na kuhamasisha wananchi kupata huduma za afya ya kinga.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Mkoyo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma Bw. Henry Kubesi amesema kuwa, yeye na uongozi wote wa Kijiji hicho wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuhakikisha Uongozi wa Ngazi ya Msingi unatambuliwa, unaheshimiwa na unashirikishwa katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Amesema kuwa, ngazi ya msingi ndio nguzo muhimu katika jamii kwa kuwa wao ndio wanawafikia wananchi kiurahisi zaidi hivyo, tunaishukuru Serikali kwa kulitambua hilo ili kuweza kuongea lugha moja ya kuleta maendeleo kwa jamii. Aidha, Bw. Kubesi ameahidi kuwa yeye akipewa ajenda ya afya huwa anahakikisha mara moja anaanza utekelezaji kwa kuwashirikisha Wenyeviti wa Vitongoji vyote 8 vya Kijiji chake ili waelewe na kupeleka ujumbe husika kwa wananchi.

Naye mhamasishaji wa afya ngazi ya jamii Bi. Anastazia Konyanza amesema kuwa yeye ni mtaalamu anayehusika na eneo la uelimishaji na uhamishaji wa wananchi hivyo, atashirikiana na wataalamu wengine wote kuhakikisha wanaendelea kuhamasisha na kuelimisha jamii yote ya Kijiji cha Mkoyo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhusu masuala yote muhimu ya afya kama ambavyo wamekuwa wakifanya na kupata ufanisi mkubwa ikiwemo kwenye eneo la Bima ya Afya ya Jamii.

Aidha katika ziara hiyo Dkt. Dorothy Gwajima aliambatana na wataalam  wa afya kutoka Wizara, Mikoa  na Halmshauri ya Jiji la Dodoma.  

 Na. Angela Msimbira HOMBOLO



Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.