logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Serikali kujenga na kukarabati shule ya msingi Kakoyoyo

Na OR-TAMISEMI, Geita

Serikali imeahidi kuanza ukarabati na ujenzi wa majengo ya Shule ya Msingi Kakoyoyo, ambayo ilifungwa baada ya baadhi ya majengo yake kutitia, kupata nyufa, na kuanguka kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mapema 2024 katika Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita.

Shule hiyo, iliyojengwa kwa nguvu za wananchi mwaka 1999, ilihudumia wanafunzi 934 ambao kwa sasa wamelazimika kusoma katika Shule ya Msingi Igwamanoni kwa kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 13.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, ametembelea shule hiyo na kuthibitisha kuwa serikali itaanza ukarabati mara baada ya tathmini ya wataalamu kukamilika.

“Tumeona uhitaji mkubwa wa kurejesha shule hii, na kupitia mapato ya ndani, serikali kuu, pamoja na wadau wa maendeleo, tutahakikisha ukarabati unafanyika ili wanafunzi waendelee kusoma katika mazingira bora,” amesema.

Naye, Diwani wa Kata ya Bulega, Mhe. Erick Kagoma, ameipongeza serikali kwa hatua hiyo, akieleza kuwa kurejeshwa kwa shule hiyo kutapunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.

Ziara hiyo imefanyika kufuatia ombi la Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ili kuwapa wananchi taarifa kuhusu hatua za serikali katika kuboresha shule hiyo.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora