
RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ametoa muda wa wiki mbili kwa uongozi wa wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga eneo la kariakoo kuanza kufungua njia ili kuruhushu shughuli za kibiashara kufanyika kwa ufanisi wakati serikali ikielekea kufanya uzinduzi wa soko jipya la Kariakoo
Akizungumza Dar es Salaam Mei 28,2025 na waandishi wa habari RC Chalamila amesema wakati maandalizi ya uzinduzi wa soko jipya yakiendelea ni muhimu Machinga Kariakoo kufungua njia za kuingia ili kupeleka bidhaa kwenye soko jipya la Kariakoo.
"Soko limeshakamilika kwa asilimia 98 hivyo natoa muda wa wiki mbili kuanzia leo Mei 28,2025 Machinga waliopo barabarani Kariakoo wakaondoka kwenda maeneo waliyopangiwa" alisisitiza Chalamila.
Kuhusu wafanyabiashara waliokuwepo kwenye Soko la Kariakoo awali kabla halijaungua Chalamila alisema wote waliokuwepo kuhakikiwa na watarejeshwa kama ambavyo Rais Dkt Samia alivyoelekeza na watapaswa kujaza mikataba,kulipa kodi na kwamba Mkoa huo umefanikiwa kuondoa udalali wa upangishaji maeneo kwa kutuia mfumo wa kidijitali wa TAUSI.
Kwa upande wake Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo Ashraph Abdulkarim alisema Shirika hilo linaendelea kuratibu wafanyabiashara waliokuwepo kurejea kwenye Soko hilo kulingana na mpangilio wa biashara.
Abdulkarim aliongeza kusema idadi ya wafanyabiashara 1150 kati ya 1520 waliohakikiwa tayari wamesajiliwa kwenye mfumo wa TAUSI ili kurejea sokoni na kuwa maeneo mengine ya wazi yaliyobaki yatatangazwa kupitia mfumo huo ili yapate wapangaji wapya.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




