logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

RC CHALAMILA ATAKA MACHINGA KARIAKOO KUFUNGUA NJIA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  Albert Chalamila ametoa muda wa wiki mbili kwa uongozi wa wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga eneo la kariakoo kuanza kufungua njia ili kuruhushu shughuli za kibiashara kufanyika kwa ufanisi wakati serikali ikielekea kufanya uzinduzi wa soko jipya la Kariakoo

Akizungumza  Dar es Salaam Mei 28,2025 na waandishi wa habari  RC Chalamila amesema wakati maandalizi ya uzinduzi wa soko jipya yakiendelea ni muhimu  Machinga Kariakoo kufungua njia za kuingia ili kupeleka bidhaa kwenye soko jipya la Kariakoo.

"Soko limeshakamilika kwa asilimia 98 hivyo natoa muda wa wiki mbili kuanzia leo Mei 28,2025 Machinga waliopo barabarani Kariakoo wakaondoka kwenda maeneo waliyopangiwa" alisisitiza Chalamila.

Kuhusu wafanyabiashara waliokuwepo kwenye Soko la Kariakoo awali kabla halijaungua Chalamila alisema wote waliokuwepo kuhakikiwa na watarejeshwa kama ambavyo Rais Dkt Samia alivyoelekeza na watapaswa  kujaza mikataba,kulipa kodi na kwamba Mkoa huo umefanikiwa kuondoa udalali wa upangishaji maeneo kwa kutuia mfumo wa kidijitali wa TAUSI.

Kwa upande wake Meneja Mkuu Shirika la Masoko Kariakoo Ashraph Abdulkarim alisema Shirika hilo linaendelea kuratibu wafanyabiashara waliokuwepo kurejea kwenye Soko hilo kulingana na mpangilio wa biashara.

Abdulkarim aliongeza kusema  idadi ya wafanyabiashara 1150 kati ya 1520 waliohakikiwa tayari wamesajiliwa kwenye mfumo wa TAUSI ili kurejea sokoni na kuwa maeneo mengine ya wazi yaliyobaki yatatangazwa kupitia mfumo huo ili yapate wapangaji wapya.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora