
Mhandisi Mativila aridhishwa Utekelezaji wa Miradi ya Barabara ya Mtili-Ifwagi na Sawala-Iyegeya
Iringa
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila ametembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa barabara za Mtili–Ifwagi na Sawala-Iyegeya, ambapo ameonesha kuridhishwa na miradi hiyo.
Barabara hizo zinazojengwa na TARURA kwa lengo la kurahisisha usafirishaji wa mazao ya chai, misitu, mbogamboga na mazao mengine kufika sokoni kwa wakati.
Amesisitiza kuwa serikali itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana huku akitoa wito kwa wakandarasi kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia muda uliopangwa.
Wananchi nao wametoa pongezi kwa serikali kwa kuwaletea maendeleo yanayoonekana na yanayogusa maisha yao ya kila siku.
Barabara hizo zinatarajiwa kurahisisha usafiri, kukuza biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma muhimu kama afya na elimu katika maeneo ya vijijini.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




