logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Mhandisi Mativila aridhishwa Utekelezaji wa Miradi ya Barabara ya Mtili-Ifwagi na Sawala-Iyegeya

Iringa

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila ametembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa barabara za Mtili–Ifwagi na Sawala-Iyegeya, ambapo ameonesha kuridhishwa na miradi hiyo.

Barabara hizo zinazojengwa na TARURA kwa lengo la kurahisisha usafirishaji wa mazao ya chai, misitu, mbogamboga na mazao mengine kufika sokoni kwa  wakati.

Amesisitiza kuwa serikali itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana huku akitoa wito kwa wakandarasi kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia muda uliopangwa.

Wananchi nao wametoa pongezi kwa serikali kwa kuwaletea maendeleo yanayoonekana na yanayogusa maisha yao ya kila siku.

Barabara hizo zinatarajiwa kurahisisha usafiri, kukuza biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma muhimu kama afya na elimu katika maeneo ya vijijini.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora