logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

Mchengerwa: daraja la muhoro ni mkombozi kwa wananchi rufiji

Na OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema ujenzi wa Daraja la Muhoro utaleta ukombozi kwa wananchi wa Kata ya Muhoro, ambao kwa muda mrefu wamekumbwa na changamoto za usafiri na hata kupoteza maisha wanapovuka Mto Rufiji.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Mhe. Mchengerwa amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mradi huo wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya Sh.Bilioni 17.

“Nimeridhishwa na kasi ya ujenzi, lakini nataka mkandarasi aongeze juhudi ili daraja likamilike ifikapo Julai 2025,” amesisitiza Waziri Mchengerwa.

Kwa mujibu wa Meneja wa Wakala qa Barabara Mijini na Vijijiji (TARURA) Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold Runji, ujenzi umefikia asilimia 40, tayari nguzo nne kati ya sita zimekamilika na lina urefu wa mita tisa, hivyo litasaidia kuzuia mafuriko.

Nao, Wakazi wa Muhoro, Pili Lwambo na Mikidadi Omary, wameeleza furaha yao, wakisema daraja hilo litaepusha vifo vinavyosababishwa na mamba, kusaidia kina mama kujifungua hospitalini, na kurahisisha usafiri wa watoto kwenda shule.
 

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora