
Mchengerwa: daraja la muhoro ni mkombozi kwa wananchi rufiji
Na OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema ujenzi wa Daraja la Muhoro utaleta ukombozi kwa wananchi wa Kata ya Muhoro, ambao kwa muda mrefu wamekumbwa na changamoto za usafiri na hata kupoteza maisha wanapovuka Mto Rufiji.
Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Mhe. Mchengerwa amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha mradi huo wa kisasa wenye thamani ya zaidi ya Sh.Bilioni 17.
“Nimeridhishwa na kasi ya ujenzi, lakini nataka mkandarasi aongeze juhudi ili daraja likamilike ifikapo Julai 2025,” amesisitiza Waziri Mchengerwa.
Kwa mujibu wa Meneja wa Wakala qa Barabara Mijini na Vijijiji (TARURA) Mkoa wa Pwani, Mhandisi Leopold Runji, ujenzi umefikia asilimia 40, tayari nguzo nne kati ya sita zimekamilika na lina urefu wa mita tisa, hivyo litasaidia kuzuia mafuriko.
Nao, Wakazi wa Muhoro, Pili Lwambo na Mikidadi Omary, wameeleza furaha yao, wakisema daraja hilo litaepusha vifo vinavyosababishwa na mamba, kusaidia kina mama kujifungua hospitalini, na kurahisisha usafiri wa watoto kwenda shule.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
ADDITIONAL BEST INDICATORS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI KADA YA ELIMU MRADI WA GPE - TSP
ORODHA YA WALIMU WALIOCHAGULIWA NAFASI ZA KUJITOLEA SHULE ZA MSINGI MRADI WA GPE TSP
BASIC EDUCATION STATISTICS 2025
TANGAZO LA KUITWA KAZINI AJIRA YA MKATABA PROGRAMU YA TIMCHIP
Habari na Matukio
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.




