logo

TAMISEMI

Students

FR
Fred Kibanofred.kibano@tamisemi.go.tz

“Marufuku malori kupita barabara za Mwendokasi” Mhe. Mchengerwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Machi 21, 2025 amekemea uharibifu wa barabara unaofanywa na Magari Makubwa (Malori) kupita Mwendokasi huku akizitaka Halmashauri na Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kufikiri namna bora ya kumaliza foleni ndani ya Dar es Salaam.

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya Utiaji Saini wa Zabuni 9 zilizobeba thamani ya Shilingi Bilioni 221.8 zinazojumuisha Barabara zenye urefu wa Kilomita 84.4 zinazotarajiwa kwenda kuboreshwa katika Halmashauri za Dar es Salaam chini ya Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP TWO).

Akizungumza wakati wa Hotuba yake Mhe. Mchengerwa amesema Mhe. Rais hatamani kuona foleni, Halmashauri kaeni fikirini namna ya kumaliza foleni ndani ya Jiji hili, mmetoa Kibali Magari kupita Mwendokasi afadhali kwa Magari madogo lakini sasa yanapita mpaka malori, barabara zimeanza kuharibika. Malori kuanzia sasa nisisikie yamekatisha ndani ya barabara za Mwendokasi.

Lakini pia tutakwenda kufanya mapitio hii asilimia ya makusanyo ya mapato ya ndani inayopaswa kwenda kwenye barabara isiwe 10% ili muifanye TARURA iwe na uwezo wa kufanya kazi masaa 24 kusimamia ujenzi wa barabara katika maeneo yetu.

Nendeni mkafungue barabara ambazo watu wanapaswa kupita kumaliza foleni, TARURA mkoa nendeni mkafikiri nini kifanyike ili mtengeneze barabara za kimkakati zinazoweza kupunguza foleni".

Mhe. Mchengerwa ameshuhudia Utiaji Saini wa Mikataba ya Ujenzi wa Barabara kupitia DMDP zenye urefu wa Km. 84.4.

Comments

Please sign in to leave a comment.

Matangazo Muhimu

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Habari na Matukio

Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.

Cookie

We use cookies to enhance your browsing experience, provide personalized content, and analyze our traffic. By clicking "Accept All Cookies", you agree to the storing of cookies on your device to improve site navigation, analyze site usage, and assist in our marketing efforts. To learn more about how we use cookies and to manage your preferences, please visit our Cookie Policy.
National Election Commission Logo

Uchaguzi 2025

Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora