• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Waziri Mkuu kufungua mashindano ya FEASSSA kesho jijini Arusha

Imewekwa tar.: August 15th, 2019

Na Mathew Kwembe, Arusha

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mashindano ya Michezo ya shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSA) utakaofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Jumla ya wanamichezo 3500 kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, wenyeji Tanzania bara na Zanzibar pamoja na nchi ya Malawi ambayo imealikwa watashiriki michuano hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Arusha Mratibu wa Mashindano hayo bwana Leonard Thadeo amesema kuwa ufunguzi rasmi utafanyika kesho saa 8.00 mchana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo utachezwa mchezo mmoja wa ufunguzi wa mashindano hayo kati ya timu ya soka ya Lindi dhidi ya timu ya St. Mary’s kutoka Uganda.

 “Tayari timu nyingi zimekwishawasili, Uganda waliwasili jana, na nimeambiwa timu kutoka Rwanda jana walilala Singida na kwa ujumla maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo yamekamilika,” amesema.

Mratibu huyo ameitaja michezo itakayoshindaniwa kwenye michuano hiyo kuwa ni pamoja na Soka, riadha, netiboli, mpira wa mikono, mpira wa mikapu, vinyoya, raga, mpira wa magongo, mpira wa meza, mpira wa kengele na michezo mingineyo.

Michezo hiyo imepangwa kuchezwa kuanzia kesho tarehe 16 agosti na fainali za michuano hii inatarajiwa kufanyika tarehe 24 agosti, 2019.

Bwana Thadeo amevitaja viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano hiyo kuwa ni pamoja na uwanja wa Magereza, Sheikh Amri Abeid, ISM, St. Constantine, TGT na ukumbi wa michezo wa Paloti.

Wakati huo huo semina ya siku tatu kwa walimu wa michezo wa shule mbalimbali nchini iliyokuwa ikifanyika katika ukumbi wa shule ya St Patrick ya jijini Arusha imefungwa rasmi leo na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania bwana Leodger Tenga.

Akizungumza mara baada ya kufunga semina hiyo ambayo iliwahusisha wakufunzi kutoka chuo kikuu cha Tsukuba cha nchini Japan, bwana Tenga amesema kuwa wamefundisha mambo mengi yakiwemo utawala, mbinu za michezo, afya za michezo pamoja na namna wanamichezo wanavyoweza kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya.

Pamoja na kuwashukuru wakufunzi hao, bwana Tenga amesema kuwa kozi za namna hiyo ni vizuri zikafanyika mara kwa mara kwani dunia imebadilika, michezo siyo tu inafanikiwa kwa kutaka, lazima kuhakikisha kuwa kuna mbinu sahihi, vifaa sahihi na wataalamu sahihi wa michezo.

Amesifu kuwepo kwa ushirikiano baina ya chuo kikuu cha Tsukuba na Tanzania katika kuendeleza sekta ya michezo ambapo chimbuko la ushirikiano huo limetokana na mahusiano baina ya Mratibu wa Michezo kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Leonard Thadeo ambaye aliwahi kusoma katika chuo kikuu cha Tsukuba cha nchini Japan.

Bwana Tenga amesema kufuatia kuimarika kwa ushirikiano huo wamewaomba wakufunzi hao wawe wanakuja mara kwa mara nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya aina kama hiyo kwani mahitaji ya mafunzo bado ni makubwa sana.l

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.