• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Wauuguzi Malampaka wasitishiwa safari za nje ya kituo

Imewekwa tar.: June 21st, 2019

Mratibu wa Mradi wa  Afya  ya Uzazi na Mtoto RMNCH-UNFPA na Huduma za Uuguzi na Ukunga  kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bi.  Dinah Atinda amesitisha safari za nje ya kituo, mikutano, semina  na likizo kwa muda wa mwezi mmoja  kwa wauguzi wa Kituo cha Afya cha Malampaka katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Mkoani Simiyu.

Ametoa maagizo mara baada yakutembelea kituo hicho na kukuta huduma za afya zikiwemo za akina mama kujifungua zikifanywa na wahudumu wa afya (Medical Attendant) wakati wauguzi wote wakiwa kwenye semina  na mikutano mbalimbali jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa majukumu ya kazi.

“Ni hatari sana muhudumu wa afya (Medical Attendant) kuwahudumia wagonjwa akiwa peke yake bila usimamizi wa muuguzi kwa kuwa anaweza kusababisha madhara au kifo kwa mgonjwa na kushindwa kutoa maelezo sahihii juu ya chanzo cha kifo hicho” Amesema Bi. Atinda.

Bi. Atinda amefafanua kuwa jukumu la kuwahudumia wagonjwa katika Zahanati na Vituo vya afya ni la Wauguzi na Madaktari na si kazi ya wahudumu wa afya hivyo wanawafanya kutotimiza majukumu yao ya kufanya usafi wa mazingira na majengo.

Ameendelea kusema Serikali imetumia fedha nyingi katika kutengeneza miundombinu ya afya na vifaa na vifaa tiba  hivyo ni muhimu kila mmoja katika nafasi yake akatimiza majukumu ya kazi aliyopangiwa ili kutimiza lengo la kutoa huduma bora kwa jamii.

Amesema wauguzi ni kada  muhimu  na asilimia zaidi ya 80 ya huduma za afya nchini zinatolewa na wauguzi hivyo ni vyema wakafanyakazi  kwa weledi na kwakufuata misingi ya taaluma yao ili kutoa bora na kupunguza vifo vinavyoweza kuzulika kwa jamii.

“Wauguzi mnao wajibu wa kutoa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia kiapo na miiko ya taaluma yenu. Tunazo taarifa kuhusu baadhi ya wauguzi kutoa lugha chafu kwa wagonjwa, kutokuwepo kazini bila taarifa, kutokupanga utaratibu wa kazi (Roster) unaozingatia miongozo na kuwapanga wahudumu wa afya zamu bila wauguzi wenye ujuzi suala hili halikubaliki” Amesisitiza Bi. Atinda

Amesisitiza inasikitisha Kituo cha afya cha Malampaka kina watumishi 23 lakini  waliokutwa kazini ni 7 wwengine wakiwa kwenye ziara, mafunzo, semina na mikutano, hivyo kuzorotesha utoaji wa huduma za afya kwa jamii.

Wakati huohuo Bi. Atinda amesitisha safari, semina  mikutano na likizo  kwa muda wa mwezi mmoja  kwa Muuguzi Mkuu wa Mkoa, Muuguzi Mkuu wa Wilaya ya Maswa  na Mratibu wa afya ya uzazi na Mtoto wa Mkoa na Wilaya  na kuwataka kusimamia na kutatua changamoto zilizopo katika kituo hicho.

Amezitaka Timu za usimamizi wa Huduma za Afya za Mikoa na Wilaya  kuhakikisha  wanatimiza majukumu yao kwa kusimamia ujenzi wa vituo viwili vitakavyojengwa na kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya  vilivyojengwa katika Mkoa wa Simiyu  vinaanza kufanyakazi.

Aidha amewataka waganga wafawidhi wa vituo kuhakikisha wanasimamia usafi, utendaji kazi na uwajibikaji wa watumishi ili vituo vya kutolea huduma za afya nchini vinaboreka na kuwavutia wananchi kuja kupata huduma hiyo.

Anaandika Angela Msimbira MASWA







Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha nusu Mwaka (Julai – Disemba, 2019) kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 February 09, 2020
  • Tangazo la kazi kada ya Afya January 20, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • “PS3 plus” Yarudi kwa kishindo, Bilioni 114 kuwezesha Mifumo Sekta ya umma nchini

    January 16, 2021
  • Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

    January 14, 2021
  • Mweli awatolea uvivu kidato cha Nne, Sita, awajenga kinidhamu

    January 11, 2021
  • Mweli awatega Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu kwenye Mfumo wa PREM/PREMS.

    January 10, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.