• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

WATANZANIA WATAKIWA KUJIUNGA NA CHF ILIYOBORESHWA

Imewekwa tar.: December 14th, 2020

Mkurugenzi wa Huduma za afya, lishe na ustawi wa jamii Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt Ntuli Kapologwe amewataka waganga wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujiunga na mfuko wa bima ya afya ilioboreshwa.

Dkt. Kopologwe ametoa wito huo leo wakati akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake juu ya uhamasishaji wa jamii kujiunga na mfuko wa bima ya afya ilioboreshwa (CHF) ili kupunguza gharama zisizo za lazima wakati wa kupata huduma za afya kwa wananchi.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo Dkt. Kapologwe ameeleza kuwa asilimia 86 ya wananchi hawajajiunga na Bima ya afya nchini kutokana na kutopata elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kuwa na bima ya afya ya jamii.

“Umuhimu wa kujiunga na bima ya afya ya jamii ni kuepuka gharama za matibabu za hapo kwa hapo katika hospitali,vituo vya Afya na zahanati zetu zilizopo nchini.

Pia amesema kuwa faida ya CHF iliyoboreshwa ni kuwa imeongeza wigo mpana wa upatikanaji wa huduma kwani ukiwa na hiyo bima popote pale ulipo nchini unaweza kupatiwa huduma za afya tofauti na awali huduma ilikuwa katika eneo ulilojiandikisha.

Hivyo taratibu za kujiunga na bima hiyo mwananchi anakwenda kujiandikisha katika ofisi za mitaa, vijiji, vitongoji na mawakala walio katika maeneo yao ili kuweza kusaidia wananchi kujiunga bila vikwazo.

“Baada ya maboresho kuna mfumo ambao unawezesha kutambua mtu wapi alisajiliwa na wapi ametibiwa na kurahisisha urejeshaji wa fedha katika kituo cha kutolea huduma husika”, ameeleza Mkurugenzi huyo.

Vile vile amesema kuwa bima ya afya iliyoboreshwa imepanua wigo wa mafao kwa kuongeza baadhi ya huduma kupatikana katika bima hiyo kama upasuaji mkubwa na mdogo.

Hivyo takribani vituo 6,000 vinauwezo wa kuwahudumia wananchi wanaojiunga na CHF iliyoboreshwa ikiwemo Zahanati 4,922, Vituo vya Afya 716, Hospitali za Wilaya 179 na Hospitali za Mikoa 28.

Aidha Dr. Ntuli aliongeza kuwa kwa upande wa ada kulifanyika utafiti kuweza kujua ni kiasi gani mwananchi anaweza kumudu ili aweze kuchangia ambapo asilimia 98 walisema wana uwezo wa kuchangia shilingi 30,000 ambapo ndicho kiasi kinachotumiwa kwa kila kaya moja ya watu wapatao sita kwa mwaka mmoja.

“Ada hiyo ni kwa maeneo yote isipokuwa Mkoa wa Dar es Salaam ambao ada yao ni shilingi laki moja na nusu kwa kaya moja yenye idadi ya watu sita na shilingi elfu arobaini kwa mtu mmoja na hii ni kutokana na wigo wa vituo vya kutolea huduma katika Mkoa huo ambapo vituo binafsi vitashirikishwa katika utoaji wa huduma ”,amesisitiza .

Pia amesema kuwa mwananchi akiwa amechangia kiasi hicho kwa mwaka na Serikali inachangia kiasi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa mwananchi.

Dkt.Kapologwe ameeleza kuwa tayari Serikali imechangia ruzuku ili kuhakikisha inaboresha huduma za mfuko wa bima ya afya ya jamii.

Mchango wa Serikali katika kuboresha huduma za afya imeboresha miundombinu kwa kujenga hospitali za wilaya mpya 102, vituo vya afya 487, zahanati 1198, ununuzi wa vifaa tiba kwa lengo la kuhakikisha huduma bora zinatolewa ili kutimiza matakwa ya wananchi.

MWISHO

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Vikundi 47 Kondoa vyapewa mikopo ya shilingi milioni 147

    February 24, 2021
  • Mikopo ya Shilingi Milioni 85 yatolewa kwa Vikundi wilayani Bunda

    February 24, 2021
  • Mradi wa Fursa na Vikwazo Iliyoboreshwa Kuingizwa kwenye Majukumu ya OR - TAMISEMI

    February 23, 2021
  • Mikopo ya Sh. Milioni 850 yatolewa kwa Vikundi 104 jijini Tanga

    February 15, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.