• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Ugatuaji wa Madaraka sasa kuwa na nguvu ya kisheria na kisera

Imewekwa tar.: April 6th, 2019

Serikali imesema Sera ya Taifa ya Ugatuaji wa Madaraka ya mwaka 2019 ambayo hivi sasa ipo katika hatua ya rasimu itakapokamilika itakuwa na nguvu ya kisheria na kisera tofauti na ile ya mwaka 1998 ambayo ilikuwa ni sera ambayo haikuwa na nguvu ya kisheria.

Hayo yameelezwa jana mjini Masasi, mkoani Mtwara na Mkurugenzi wa Idara ya huduma za Kisheria kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Edwin Mgendera mara baada ya kufunguliwa kwa kikao kazi cha kupokea maoni ya wadau juu ya rasimu ya sera ya Taifa ya ugatuaji wa madaraka ya mwaka 2019 kwa wananchi wa mikoa ya kusini ya Mtwara, Lindi na Ruvuma.

Bwana Mgendera amesema mafanikio na changamoto zilizotokana na utekelezaji wa Sera ya Ugatuaji ya mwaka 1998 imeiwezesha serikali kuja na Sera ya jumla ya ugatuaji kitaifa ambayo itakuwa na nguvu za kisheria na namna bora ya kutekeleza na kutoa huduma kwa ufanisi kwa wananchi toka juu serikalini hadi ngazi za chini za Kitongoji na Mtaa kule kwenye Halmashauri.

Amesema mwelekeo wa serikali kwa sasa ni huo wa kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Ugatuaji wa Madaraka ambayo itawekewa nguvu za kisheria na kisera ili kurahisisha suala la utoaji huduma kwa wananchi moja kwa moja kutoka serikali kuu hadi ngazi za kitongoji na mtaa.

Mkurugenzi huyo wa huduma za Sheria amefafanua kuwa Msingi wa Sera ya Taifa ya Ugatuaji wa Madaraka ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka, 1977 Ibara ya 145 na 146 ambazo zimetoa uhalali wa kuanzishwa kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na kubainisha madhumuni ya kuanzishwa kwa Mamlaka hizo yakiwemo kuzipa Mamlaka za Serikali za Mitaa madaraka ya kujiamulia mambo yao ya Maendeleo ya Kijamii na Kiuchumi katika maeneo yao kwa uhuru.

“Aidha Sheria Na. 7 ya Halmashauri za Wilaya ya mwaka 1982 (sura 287) na Sheria Na. 8 ya Halmashauri za Miji ya mwaka 1982 (sura 288) zinazipa mamlaka hizo majukumu ya kutoa huduma kwa jamii katika maeneo husika,” amefafanua bwana Mgendera.

Pia Mkurugenzi huyo ameitaja sheria ya Tawala za Mikoa ya Mwaka 1997 ambayo inazipa Tawala za Mikoa jukumu la kuratibu maendeleo katika Mikoa yao ikiwemo kuzisimamia na kuzisaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kutoa huduma bora kwa usawa kwa jamii.

Ni kutokana na msingi huo wa sheria bwana Mgendera amesema kuwa masuala ya Ugatuaji wa Madaraka yanafanyika na yataeendelea kufanyika katika hatua mbili muhimu ambazo ni kugatua Madaraka kutoka Serikali Kuu kwenda Ngazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji) na pili kugatua Madaraka kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenda ngazi za Msingi yaani Kata, Vijiji, Mitaa na Vitongoji.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Kisekta kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana Juma Idd ambaye pia ndiye Mratibu wa kikao kazi cha kupokea maoni ya wadau juu ya rasimu ya sera ya Taifa ya ugatuaji wa madaraka ya mwaka 2019 ameeleza kuwa hivi sasa timu yake ipo katika mikoa hiyo ya kusini baada ya zoezi hilo kukamilika katika mikoa ya nyanda za juu kusini ya Mbeya, Iringa, Njombe, Songwe na Rukwa.

Ameongeza kuwa baada ya kukamilika katika mikoa hiyo, timu ya kupokea maoni itaelekea katika kanda ya mashariki ambapo Mikoa ya Morogoro, Dar es salaam, Pwani na Dodoma itashirikishwa, na baadaye zoezi hilo kuhamia mikoa ya kaskazini, magharibi na kanda ya ziwa.

“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa wadau wetu muhimu wanapata fursa ya kutoa maoni yao juu ya nini wangependa kiwemo katika sera yetu hii mpya ya Ugatuaji wa Madaraka,” amesema bwana Idd.

Awali akifungua kikao kazi cha kupokea maoni Mkuu wa Wilaya ya Masasi bwana Selemani Mzee ameeleza umuhimu kikao hicho ambapo amesema kuwa toka mwaka 1998 Serikali kupitia Rasimu ya maboresho ya Serikali za Mitaa (LGRP) imekuwa ikitekeleza dhana ya ugatuaji wa Madaraka ili kufikisha na kuharakisha utoaji wa huduma za Kijami,Kiutawala na Kiuchumi kwa wananchi kwa haraka na kwa usawa.

Amesema kuwa kupitia dhana ya ugatuaji wa madaraka, wananchi wanapata fursa ya kutosha ya kushiriki na kushirikishwa katika shughuli na masuala yote yanayohusu maendeleo yao na ustawi wa maisha yao.

Miongoni mwa wanaoshiriki kikao hicho ni pamoja na waheshimiwa Wabunge wanaotoka Mikoa ya kusini ambapo Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mheshimiwa Hassan Elias Masala amesema kuwa kikao hicho ni muhimu kwao kama wawakilishi wa wananchi kwani utekelezaji wa ahadi nyingi za serikali kupitia chama kilichopo madarakani hivi sasa unategemea sana utekelezaji wa sera hii ya ugatuaji wa madaraka.

Naye Bi Miriam Mwaibula mshiriki kutoka asasi isiyo ya kiserikali ya TWAWEZA amesema kuwa maoni yao ni muhimu kwani yatawezesha serikali kupata sera madhubuti na ambayo itakubalika na jamii yote na hivyo kurahisisha utekelezaji wake.

Kikao hicho cha siku mbili kimewahusisha Wakuu wa Wilaya, Wabunge, Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi kutoka katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Viongozi wa dini na Washiriki kutoka Asasi za Kiraia kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, na Ruvuma.

Anaandika  Mathew Kwembe - Masasi

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.