• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Tuzo ya Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri kutolewa Juni 20 mwaka huu

Imewekwa tar.: February 24th, 2019


Na Mathew Kwembe, Dodoma

Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania ALAT imesema kuwa inatarajia kumtangaza Meya au Mwenyekiti wa Halmashauri itakayofanya vizuri katika hafla ya utoaji wa tuzo hiyo kwa mwaka huu itakayofanyika tarehe 20 juni, 2019 huko jijini Mwanza.

Kaimu Katibu Mkuu wa ALAT Taifa bwana Abdallah Ngodu alieleza jana kuwa lengo ni kuzipongeza halmashauri zilizofanya vizuri lakini pia kuzibaini halmashauri zilizofanya vibaya ili kuangalia namna ya kuzisaidia halmashauri hizo ili nazo zifanye vizuri.

Alisema kuwa ALAT itaangalia njia mbalimbali ya kuzisaidia halmashauri zitakazobainika kufanya vibaya ikiwemo kuzijengea uwezo kwa njia ya mafunzo ili nazo ziweze kufanya vizuri miaka ijayo.

“Kwa halmashauri ambazo hazifanyi vizuri tutazibainisha na tutataka kujua kwa nini hazifanyi vizuri na tukishajua sababu tuweze kutengeneza afua za kuzinyanyua hizi halmashauri ambazo hazifanyi vizuri ili nazo zifanye vizuri,” alisema

Aliongeza kuwa halmashauri zitapimwa kwa vigezo mbalimbali mathalani kama halmashauri ili kuwa imelenga kukusanya kiasi cha bilioni nne badala yake ikakusanya bilioni moja tutataka kujua kwa nini haikuweza kufikia malengo yake.

“Sisi ALAT tutatumia kigezo cha kufikia malengo ya halmashauri na ndiyo suala ambalo mara kwa mara limekuwa likisisitizwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo kwa nini malengo hayakufikiwa, kwa hiyo tunaangalia tatizo ni nini? Ni uongozi au ukosefu wa ubunifu,” alisema na kuongeza:

“Tuzo ya viongozi wa serikali za Mitaa inaangalia pia namna halmashauri zilivyo na ubunifu katika utoaji wa huduma kwa wananchi na ukusanyaji wa mapato,” alisisitiza bwana Ngodu.

Alisema ALAT kwa kushirikiana na wadau wakishabaini tatizo uangalia namna ya kulitatua, mathalani kama tatizo ni mafunzo huangalia namna ya kutoa mafunzo kwa viongozi ili kuwajengea uwezo na kama tatizo ni uongozi kama kuna uwezo wa kubadilisha mfano watendaji wataishauri serikali ifanye hivyo lakini kwa upande wa viongozi wa kisiasa kama madiwani wataona namna ya kuwapa mafunzo.

Bwana Ngodu alisema ALAT inataka halmashauri zote 185 nchini ziwe na uwezo wa kujiendesha zenyewe kimapato badala ya kutegemea kwa zaidi ya asilimia 90 mapato ya serikali kuu.

Aliongeza kuwa lazima kiwango cha chini kilichowekwa kwa halmashauri kifikiwe ndiyo malengo makuu ya tuzo hii.

Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa tuzo hizo kutolewa kwani mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2015 wakati tuzo hizo zilipoanza kutolewa ambapo mshindi alikuwa Manispaa ya Kinondoni.

Mara ya pili tuzo hizo zilitolewa mwaka 2016 ambapo tuzo hiyo ilichukuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, iliyopo mkoa wa Shinyanga.

“Mwaka huu itakuwa ni mara ya tatu kuitoa tuzo hiyo ambapo halmashauri itakayoibuka mshindi wa jumla tutaizawadia tuzo hiyo,” alisema

Aliongeza kuwa mbali na halmashauri itakayoshinda tuzo ya jumla pia kutakuwa na zawadi kwa makundi manne ya halmashauri za Majiji, Manispaa, Halmashauri za Miji na Halmashauri za Wilaya.



Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.