• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

TAMISEMI QUEENS YAPANIA KUFANYA MAKUBWA LIGI DARAJA LA KWANZA NETIBOLI TANZANIA BARA

Imewekwa tar.: September 3rd, 2019

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Timu ya netiboli ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI QUEENS’ imejigamba kufanya vizuri katika michuano inayoendelea ya netiboli ligi daraja la kwanza inayoendelea katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Tayari timu hiyo imeshinda michezo minne kati ya sita iliyokwishacheza na  hivi sasa inashika nafasi ya pili mbele ya vinara timu ya Mbweni JKT kutoka jijini Dar es salaam.

TAMISEMI QUEENS imekwishazifunga timu za Cocacola,Jiji la Dodoma, Jiji la Tanga na SMART na imepoteza michezo miwili hadi sasa ambayo ni ya Mbweni JKT na Jiji la Arusha.

Akizungumzia michuano hiyo kocha wa timu hiyo Maimuna Kitete amesema kuwa timu yake ina nafasi nzuri ya kushiriki ligi ya muungano kutokana na maandalizi mazuri ambayo timu yake imeyafanya.

Amesema kufikia sasa timu yake imeonyesha upinzani mzuri dhidi ya timu tishio kama Mbweni JKT na ameahidi kuzichapa timu zote tatu zilizosalia katika michuano hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa timu hiyo Doto Bintaraba amesema kuwa timu ya ‘TAMISEMI QUEENS’ ina uhakika wa kushika nafasi tatu za juu kutokana na kuwaandaa vijana wake kufanya makubwa katika michuano ya ligi daraja la kwanza inayoendelea jijini Dodoma.

Amesema ari kubwa waliyo nayo wachezaji wake imempa imani ya kuendelea kufanya vizuri katika mechi tatu zilizosalia.

Naye mchezaji Lilian Jovin ambaye ndiye mfungaji tegemeo wa ‘TAMISEMI QUEENS’ amesema kuwa timu yake inaendelea kuimarika siku hadi siku na akaahidi kufanya vizuri katika michuano iliyobaki ya ligi daraja la kwanza.

Amesema kuwa kufikia sasa timu yake haiwaogopi timu yoyote na akawatahadharisha timu pinzani watakazokutana nazo wajipange kupata kipigo kitakatifu.

Kauli ya Lilian iliungwa mkono na mchezaji mkongwe wa timu hiyo Flora Odilo ambaye aliahidi ushindi mnono kwenye michezo mitatu iliyosalia katika michuano ya ligi hiyo.

‘TAMISEMI QUEENS’ imebakiza mechi dhidi ya Eagle, JKT Makutupora na JKT Mbweni.

Hadi sasa wanaoongoza ligi hiyo ni timu ya JKT Mbweni yenye pointi 10, ikifuatiwa na ‘TAMISEMI QUEENS’ikiwa na pointi 8, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na timu ya JKT Makutupora iliyo na pointi 8 pia huku nafasi ya nne na ya tano zikichukuliwa na timu za Jeshi Stars na Jiji la Arusha.

Mbali na michuano hiyo kutoa bingwa wa mchezo wa netiboli Tanzania Bara, timu sita za juu zitafanikiwa moja kwa moja kushiriki ligi ya netiboli ya muungano iliyopangwa kufanyika mjini Zanzibar baadaye mwaka huu.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.