• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Shirika la Elimu Kibaha watakiwa Kujiimarisha Kiuchumi

Imewekwa tar.: May 28th, 2020

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo ameiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Elimu Kibaha kutumia rasilimali za shirika kujiimarisha kiuchumi.

Jafo alitoa agizo hilo jana jijini hapa wakati wa kuzindua bodi mpya ya Shirika hilo inayoongozwa na Profesa Raphael Chibunda.

Alisema Shirika limekuwa na rasilimali nyingi ikiwamo ukubwa wa ardhi ambao kama bodi itafanya ubunifu itaweza kuitumia kufanya uwekezaji wenye tija utakaosaidia shirika kujiimarisha kiuchumi na kujitegemea.

Hata hivyo katika kutekeleza hilo, Jafo alionya uongozi wa shirika na bodi ya shirika hilo kuwa makini na uwekezaji ambao wataamua kuufanya na kusisitiza kuwa ni lazima kuwe na uwekezaji wenye tija ambao utakuwa na manufaa.

“Shirika la Elimu Kibaha lina ardhi kubwa sana, ambayo kama mtakuwa wabunifu mtakuja na uwekezaji ambao utasaidia sana kuimarisha uchumi wa shirika, mnaweza kuja na maduka ya kisasa pale.

“ Lakini nitoe angalizo, ni lazima uwekezaji mtakaoamua kuufanya muwe makini kwa kuwa na uwekezaji wenye tija, maana kunawatu wajanja wanaweza kuja na maandiko yao feki na kufanya uwekezaji ambao hauna tija.”

Aidha, Jafo alisema ni vyema Bodi hiyo ikaandeleza na kuchagiza maono ya Baba wa Taifa, Julius Nyerere ambaye aliamua kuanzisha Shirika hilo ili kupambana na maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umasikini.

Jafo pia aliitaka Bodi kuhakikisha inaimarisha taasisi za shirika hizo kama hospitali ya Tumbi, chuo na shule zilizo chini ya Shirika ili ziendelee kufanya vizuri na kuwanufaisha wananchi wanaozunguka shirika na watanzania kwa ujumla.

Jafo pia alilipongeza Shirika hilo kwa Hospitali ya Tumbo kuja na ubunifu wa kutengeneza maji tiba(drip) ambao umesaidia kuipunguzia serikali gharama za kuagiza maji hayo sambamba na shule ya sekondari kibaha na Chuo cha Ufundi (TDF) kufanya vizuri.

MKuu wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Bodi alisema changamoto inayofanya Shirika hilo kutosonga mbele ni ufinyu wa bajeti.

Mshana ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa bodi iliyopita aliomba serikali kuhakikisha inatoa majibu ya kuruhusu au kukataa maandiko mradi ambayo Shirika inaomba kutekeleza kwa haraka ili kuweza kusonga mbele.

“Tumekuwa tunakwama sana kutokana na kuchelewa kwa serikali kutoa kauli ya ndio au hapana katika maandiko mradi ambayo Shirika tumekuwa tukiomba kutekeleza.

“ Unapeleka andiko, mwaka mmoja, miwili hupati jibu lakini tukipata majibu mapema ya kama ndio tuendelee au hapana inakasoro badilisheni hili na lile, au mradi huu haufai kabisa ili kuja na mawazo mengine, hivyo tunawaomba wataalamu wa TAMISEMI kufanyia kazi maandiko tunayowaletea.”

Naye Mwenyekiti wa Bodi, Profesa Chibunda alisema Bodi yake inakwenda kutekeleza maagizo aliyoyatoa na kulifanya shirika liimarike zaidi.

Pia alioamba ushiriki wa karibu wa Shirika katika hospitali ya Tumbi na Shule zake ambavyo kwa sasa viko chini ya Serikali.

“Tunaona kuna haja ya kubadilishwa kwa mfumo wa uendeshaji, tunataka  ya shirika kwenye shule, hopitali ya Tumbi ili Shirika liweze kuwekeza.”

Shirika la Elimu Kibaha ni Shirika la umma linalotoa huduma mbalimbali, lililopo Mkoa wa Pwani, lilianzishwa mwaka 1963 kama mradi wa pamoja chini ya wafadhili watano- Serikali ya Tanganyika kwa kipindi hicho kwa upande mmoja pamoja na nchi nne za Kinordic (Dernmark, Norway, Finland na Sweden) kwa upande mwengine.

Kwa kipindi hicho mradi huu ulijulikana kama “Tanganyika Nordic Project” mpaka mwaka 1970 ambapo mradi huu ulikabidhiwa rasmi kwa Serikali ya Tanzania na kuitwa Shirika la Elimu Kibaha. Na kusajiwa chini ya sheria ya Mashirika ya Umma Na.17 ya mwaka 1969, marejeo ya mwaka 2002.


 

Na. Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.