• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

Imewekwa tar.: January 14th, 2021

Na Atley Kuni, Dodoma

Serikali imetoa vifaa na visaidizi maalum vya aina mbalimbali vyenye thamani ya Shilingi bilioni 3 kwa ajili ya wanafunzi 18,488, ambao wana mahitaji maalum wa shule za msingi na sekondari nchini ili kuwawezesha wanafunzi hao kumudu masomo katika shule zao.

Akizindua zoezi la usambazaji wa vifaa hivyo leo mjini Dodoma, Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo, amesema, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Programu ya EP4R imeweza kununua jumla ya vifaa na visaidizi maalum 51,339 vya aina mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum wa shule za msingi na sekondari.

Amesema kuwa Vifaa hivi vilivyonunuliwa vimegharimu jumla ya Shilingi 2,833,374,280 na vitasambazwa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum ambao wamegawanyika kwenye makundi maalum yapatayo manane.

Waziri Jafo ameyataja makundi hayo ya wanafunzi wenye mahitaji maalum kuwa ni Viziwi, Wasioona, Albino, Wenye Uoni Hafifu, Wenye Ulemavu wa Viungo, Wenye Ulemavu wa Akili, Wenye Usonji na Wenye Uziwi na kutokuona.

Amesema shabaha ya Serikali ni kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wanapata elimu iliyokusudiwa ikiwa ni mpango wa utekelezaji wa sera ya Elimu ya mwaka 2014.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI imeweka mkazo katika kukabiliana na vikwazo dhidi ya uwepo ushiriki na ujifunzaji kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. Mojawapo ya hatua ambayo imechukua ni kununua vifaa maalum vya kielimu na visaidizi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum,” amesema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga, amesema, katika kipindi cha miaka mitano, 2016/2020 cha Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefanya mambo mengi katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum ikiwemo kuongezeka kwa shule zinazo wahudumia wanafunzi wa Elimu ya Awali, zilizoongezeka kwa asilimia 46.1, msingi asilimia 23.9 na Sekondari 24.6.

“Mheshimiwa Waziri mbali na hayo, ongezeko la Watoto wenye mahitaji maalum walioandikishwa ni asilimia 46.1 kwa elimu ya awali, asilimia 34.0 kwa elimu ya msingi na asilimia 74.6 ni kwa sekondari,” alisema Nyamhanga.

Katibu Mkuu ameongeza kuwa, wanafunzi wenye Ulemavu wanaohitimu Elimu ya Msingi na kujiunga na Sekondari imeongezeka kutoka asilimia 69.9 mwaka 2016 hadi asilimia 76.3 mwaka 2020.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, anayeshughulikia Elimu maalum, Julius Migeha, alisema hivi sasa Serikali inaendelea na la kuwabaini watoto wenye mahitaji maalum ili waweze kuandikishwa na kupatiwa elimu, hivyo akawataka wazazi wenye watoto wa aina hiyo kutoa ushirikiano kwa timu ili dhamira ya serikali iweze kutimia.

Katika mwaka wa fedha 2017/18, serikali ilifanikiwa kuendesha utaratibu wa kuwabaini watoto wenye mahitaji maalum, ambapo jumla ya  watoto 16,436 waliweza kufikiwa na kwa mwaka huu lengo la serikali ni kuwafikia Watoto 18,000.

Ofisi ya Rais TAMISEMI inajukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa Elimu ya Awali, Shule za Msingi na Shule za Sekondari, hii ni pamoja na kuhakikisha mahitaji muhimu ya kujifunzia na kufundishia yanapatikana kwa lengo la kupata idadi kubwa ya Watanzania walioelimika na wanaopenda kujielimisha zaidi ili waweze kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa letu bila kujali tofauti zao.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Vikundi 47 Kondoa vyapewa mikopo ya shilingi milioni 147

    February 24, 2021
  • Mikopo ya Shilingi Milioni 85 yatolewa kwa Vikundi wilayani Bunda

    February 24, 2021
  • Mradi wa Fursa na Vikwazo Iliyoboreshwa Kuingizwa kwenye Majukumu ya OR - TAMISEMI

    February 23, 2021
  • Mikopo ya Sh. Milioni 850 yatolewa kwa Vikundi 104 jijini Tanga

    February 15, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.