• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Serikali Yaagiza Maafisa Elimu Mikoa na Wilaya Kusimamia Taaluma

Imewekwa tar.: February 16th, 2019

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga ameagiza Maafisa Elimu Mikoa na Wilaya kuendelea kusimamia taaluma kwa kuzingatia ufaulu wa wanafunzi pamoja na ujenzi wa miradi ya elimu na usimamizi wa fedha zote za sekta ya elimu nchini.

Mhandisi Nyamhanga ameyasema hayo wakati wa ziara yake mkoani Mwanza jana wakati akikagua miradi ya maendeleo sekta ya elimu, katika Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela ambapo akiwa katika shule ya sekondari Nyegezi na Fumagila zilizopo Jijini Mwanza na katika shule ya sekondari Kayenze na shule ya msingi Isenga D zilizopo Manispaa ya Ilemela amewaagiza watendaji hao kusimamia taaluma na kuzingatia matumizi sahihi ya fedha za elimu ili kuondokana na hoja za ukaguzi.

“Maafisa Elimu wote muendelee kusimamia ufaulu na taaluma na fedha zote za miradi ya elimu kama EP4R (Lipa Kulingana na matokeo), EQUIP T na fedha zote zinazotolewa na Serikali kila mwezi, hakikisheni zinatumika kulingana na kazi iliyopangwa na kwa kuzingatia thamani ya fedha halisi na kuepuka hoja za ukaguzi” alisema Mhandisi Nyamhanga.

Nyamhanga amesema Serikali inatoa fedha za Elimu Bila Malipo kila mwezi kiasi cha shilingi bilioni 23.7 kama sehemu ya malengo ya Serikali ya Chama Tawala kugharamia elimu ili kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wanapata elimu bila kulipia kuanzia ngazi ya chekechea, shule ya msingi hadi shule ya sekondari kidato cha nne.

Aidha, Mhandisi Nyamhanga amesema Serikali inafanyia kazi suala la ajira mpya za walimu hasa masomo ya sayansi ili kupunguza uhaba wa walimu wa sayansi na pia Ofisi ya Rais TAMISEMI itapeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 90 katika shule ya sekondari Fumagila na milioni 90 katika shule ya sekondari Nyegezi kwa ajili ya kujengea jengo la utawala.

Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Fumagila mwalimu Victor Lyambogo amesema wamepokea kiasi cha shilingi 66.3 milioni kwa ajili ya kujengea madarasa matatu na matundu sita ya vyoolakini bado wanaupungufu wa matundu 30 ya vyoo na jengo la utawala.

Doto Boki mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Nyegezi amesema bado wanakabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa, vitabu vya masomo ya sayansi na madawati kutokana na ongezeko la wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza mwaka 2019.

Lengo la ziara ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga mkoa wa Mwanza na Mara ni kujitambulisha kama Mtendaji mpya pia kufuatilia na kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na vituo vya afya, zahanati na hospitali za wilaya, ukarabati na ujenzi wa barabara zilizo chini ya TARURA na TSCP, ujenzi wa shule za msingi na sekondari.

                                       Anaandika Fred Kibano

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Bil 16.4/- zarejesha hadhi ya Shule za Sekondari za Ufundi nchini

    January 22, 2021
  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.