• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Serikali kufanya Maboresho Makubwa Mitaala ya Afya nchini

Imewekwa tar.: January 28th, 2019

Jopo la Wataalam kutoka Idara Mbali Mbali za Serikali wakiongozwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Wizara ya Afya, wanakusudia kuboresha Mitaala ya Vyuo vya elimu ya Afya huku nguvu kubwa ikielekezwa katika matumizi sahihi ya takwimu zipatikanazo kutoka katika vituo vya kutolea huduma za afya na matumizi yake.

Wadau hao waliokutana kwa siku moja mjini Morogoro, walisema kwa muda mrefu takwimu nyingi zinazopatikana kutoka katika vituo vya kutolea huduma zimekuwa zikukusanywa kwa mazoea na hivyo kubaki bila kutumika katika ngazi mbali mbali za maamuzi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa TEHAMA OR-TAMISEMI, Afisa TEHAMA, Melkiory Baltazari alisema, taaluma bora ni ile inayotafsiri maendeleo ya watu kwa vitendo na maendeleo hayo kuisaidia jamii.

“Tunazalisha data nyingi sana, lakini kiwango cha matumizi ya data hizo hakikidhi viwango tunavyo hitaji hususa ni katika ngazi za maamuzi alisema Baltazary na kuongeza kuwa, ukimfunza mtu, halafu taaluma yake hiyo ikatumika vizuri kwa kile kilicho kusudiwa utaona thamani ya elimu husika”.

Naye Mtaalam kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Issa Mbaga, alisema, umefika wakati suala la data likaingizwa katika mitaala ya vyuo vya wataalam wa Afya ili kuwajengea utamaduni wakuthamini takwimu pindi wawapo katika utekelezaji wa majuku yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa kutoa salaam za mradi wa PATH Tanzania, Mkurugenzi wa mradi wa Data Use Partnership Bi. Jackie Patrick, alisema anaipongeza Serikali kwa kuamua kuboresha suala la mifumo na matumizi ya takwimu kwa mapana yake kama yalivyoainishwa kwenya “Tanzania Digital Health Investments Roadmap 2017-2013”

“Sisi tunaipongeza sana Serikali ya awamu ya tano kwa namna inavyo weka msisitizo katika matumizi ya takwimu hususani zile tunazo zipata kutoka katika vituo vya kutolea huduma. Pia naipongeza serikali kwa kuamua kutumia ubunifu wa hali ya juu kujengea uwezo wa wahudumu wa afya kwa kuanzisha “Data Use Capacity Building Consortium” kupitia mradi wake wa Data Use Partnership ulioko chini ya wizara ya afya na Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Alisema Bi. Jackie na kuongeza kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi chache Afrika kama sio pekee inayotumia ubunifu huu wa hali ya juu wa kutumia muungano “consortium” wa taasisi za kitafiti na taasisi za mafunzo za ndani ya nchi kujenga uwezo wa wahudumu wa afya kwenye matumizi ya takwimu. Huu ni ubunifu wa gharama nafuu na wa kudumu katika sekta ya afya” alihitimisha

Kando ya mafunzo hayo yakuwajengeana uwezo wataalam hao, Mkuu wa Chuo Uuguzi Ifakara, Prof. Florah Kessi, aliwaambia waandishi wa habari kwamba, lengo la Mafunzo hayo ni kuondokana na kufanya kazi kwa mazoea.

“Katika Mpango wa sasa, tunataka watoa huduma wanao ingia vyuoni na wale waliomaliza vyuo lazima sehemu ya mitaala yao, soma la ‘data use’ lipewe kipaumbele, maana walio wengi wanakusanya data lakini hawazitumi. ” alisema Prof.  Kessy na kuongeza kuwa, mara kwa mara nimekuwa nikimsikiliza Mhe. Rais kwenye hutuba zake, kubwa analolifanya nikuongea kwa kutumia takwimu, lakini halikadhalika Mawaziri, Wabunge na viongozi wengine pia hawajaacha kutumia takwimu katika hotuba zao”.

Kwa upande wao washiriki wa semina hiyo, walisema wakati wa maboresho ya mitaala hiyo upo umuhimu wa kuwahusisha wataalam wa afya waliopo kazini ambao wana uzoefu lakini pia kutambua matumizi ya data walizo nazo.

“Tunapo andaa mitaala hii kwaajili kuiboresha mitaala yetu, tusiache kuwahusisha wakusanyaji, lakini pia watumiaji wa siku kwa siku ili kujiridhisha kwenye uhalisia wa data.” Alinikuliwa Faraja Makafu kutoka NACTE.

Akifunga Semina hiyo ya siku moja ya kujadili matokeo yaliyopatikana baada ya mchakato huo wakujadili kozi za muda mfupi na zile za muda mrefu kwa watumishi waliopo makazini na wale wanaojiunga na vyuo Mkurugenzi msaidizi wa huduma za afya Dkt. Anna Nswira kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, alisema katika hali ya sasa, mtaalam wa afya ndio Mchumi, Mwalimu, Mhandisi na ndio mwanasheria na taaluma zingine, hivyo wakati nchi inahubiri suala la uchumi wa viwanda hatutafikia huko kama wananchi watakuwa hawana afya njema.

Kukamilika kwa mtaala huo na kuanza kutumika katika vyuo vya kati na vyuo vikuu itasaidia kuimarisha matumizi ya data katika ngazi mbali mbali za maamuzi hususan wakati wa kupanga.

Anaandika  Atley Kuni- Morogoro




Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Bil 16.4/- zarejesha hadhi ya Shule za Sekondari za Ufundi nchini

    January 22, 2021
  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.