• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Rais Magufuli Aweka Jiwe la Msingi Hospitali ya Wilaya Nkasi, Afungua Kituo cha Afya Namanyere

Imewekwa tar.: October 9th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameweka jiwe la msingi katika hospitali ya wilaya Nkasi ambayo ni kati ya hospitali 67 zinazojengwa katika halmashauri mbalimbali hapa nchini na kusema Serikali ipo pamoja na watanzania katika kuboresha huduma za afya.

Pia Rais Magufuli amefungua kituo cha afya Nkomolo kilichopo wilayani Nkasi kwa niaba ya vituo vingine 9 vilivyopo katika mkoa wa Rukwa na kuwashukuru Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto na kusema kuwa Serikali itaendelea kutenga fedha katika sekta ya afya ili kuboresha afya ya watanzania, amewasihi watendaji na wanasiasa kushirikiana ili kuendelea kuboresha huduma za afya kwa manufaa ya jamii.

Rais Magufuli amesema katika mwaka huu pekee wa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 270 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa madawa kwa nchi nzima.

Aidha, amewapongeza madaktari na manesi wilayani Nkasi na nchi nzima kwa kazi nzuri wanayoifanya lakini pia ametoa shukrani za pekee kwa madaktari bingwa kutoka Italia waliokuja na kufanya kazi katika kituo cha afya Namanyere wilayani Nkasi ambapo opereshi mbalimbali ambazo hufanywa katika hospitali za rufaa zinafanyika wilayani hapo.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amefungua barabara ya Sumbawanga hadi Kanazi yenye urefu wa kilomita 75 iliyogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 91 ambazo ni fedha za Serikali na kufanya kuendelea kuboreshwa kwa barabara za ukanda wa nyanda za juu magharibi inayotarajiwa kuchochea uchumi katika eneo hilo. Rais Magufuli amewasihi wananchi kuitumia fursa ya barabara hiyo ili kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa Taifa na wananchi mmoja mmoja.

Akitoa maelezo ya awali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amesema katika histori ya Tanzania Tangu uhuru haijawahi kutokea kujengwa kwa hospitali nyingi kwa wakati mmoja kwani mpaka sasa jumla ya hospitali 69 za wilaya zinajengwa na katika mwaka wa fedha 2019/2020 zinajengwa hospitali 27 na kufanya kuwa na idadi ya hospitali 96 mpya ukilinganisha na hospitali 77 zilizokuwepo tangu uhuru.

Naye Ummy Mwalimu Waziri wa Afya, Jinsia, Wazee na Watoto amesema wilaya ya Nkasi hapo awali kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani ilikuwa ikipata kiasi cha shilingi milioni 130.4 kwa mwezi lakini kwa hivi sasa baada ya kuimarika kwa makusanyo ya mapato inapata kiasi cha shilingi 588.5 kwa mwezi ambayo ni sawa na asilimia zaidi ya 90 ya upatikanaji wa dawa na hivyo amewasihi watanzania kuendelea kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


       Anaandika Fred Kibano


Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

    March 03, 2021
  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Waziri Jafo ataka Shilingi Bilioni 245 za Miradi ya Maendeleo zitumike kwa wakati

    March 01, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.