• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

“OPRAS Iwe nyenzo ya Mikataba ya Utendaji kazi” Nzunda

Imewekwa tar.: October 30th, 2018

Mwakilishi kutoka Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za Umma PS3 anayeshughulikia 

Rasilimali watu Geoffrey Lufumbi, akitoa maelezo ya 

utangulizi juu ya madhumini ya mafunzo hayo

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia elimu Tixon Nzunda, amesema imefika wakati Mfumo wa upimaji utendaji kazi uliowazi (Open Performance Review Appraisal System-OPRAS) kutumika kama nyenzo muhimu ya upimaji kazi wenye matokeo chanya.

Nzunda amesema hayo hivi leo alipokuwa akifungua, mafunzo ya siku mbili kwa Maofisa Elimu pamoja na Makatibu wa Tume ya Watumishi wa Walimu TSD jijini Dodoma kutoka Halmashauri za Mkoa wa Singida.

“Mtumishi wa umma anatakiwa kupimwa kwa kuangalia mambo mahususi muhimu katika utendaji wake kama, umahiri wake, ubunifu wake na weledi wa kutumia taaluma yake katika utekelezaji wa majukumu yake.”

Naibu Katibu Mkuu Nzunda, alisema OPRAS isitumike kama fimbo ya kuwaadhibu watumishi bali kuwasaidia kutatua changamoto ambazo zitabainishwa kulingana na kada husika na mazingira ya utendaji kazi.

Ameongeza kuwa katika mfumo wa zamani ambao ulikuwa wa siri, ulimnyima mtumishi kujua kile kinacho jazwa na msimamizi wake wa kazi hali iliyochangia baadhi ya wasimamizi kuwaadhibu watumishi kwa hila na chuki binafsi.

“Katika mfumo wa sasa, Mwajiri/msimamizi wa kazi na mwajiriwa watakaa pamoja na kukubaliana kulingana na vigezo vilivyokubalika kupitia fomu ya OPRAS na endapo hawatakubaliana watakwenda kwa msuluhishi” alisema Nzunda na kuongeza, “inawezekana mtumishi ameshindwa kufikia malengo kwa sababu amekwamishwa na kutokuwepo kwa nyenzo lakini wewe msimamizi unataka kumuadhibu. hiyo sio sahihi”.

Naibu Katibu Mkuu, amewataka Maafisa Elimu hao kukubali kubadilika na kuachana na dhana za kizamani za kuishi katika mifumo ya kizamani na badala yake wapokee mawazo chanya yatakayo saidia katika utendaji kazi.

Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu Nzunda ametumia fursa hiyo kuwaonya watumishi walimu walio wezi wa mitihani na wale watakao bainika kufanya hivyo hatakuwa na simile nao.

“Tunataka kujenga heshma ya nchi, tunapojenga heshima ya nchi lazima suala la elimu lipewe kipaumbele muhimu, hatuwezi kuwafundisha watoto wetu kuwa wezi kuanzia darasa la saba halafu tunataka waingie katika soko la ushindani kimataifa hatutaweza”, alisisitiza Nzunda.

Nzunda ameahidi kulisimamia suala la wizi wa mitihani kwa juhudi zake zote na katika kipindi chake chote katika nafasi yake hiyo hatakuwa tayari kuona kadhia hiyo inajitokeza nakusema yeyote atakaye thubutu hatavumiliwa, sheria za kazi zitachukuliwa ikiwepo kufikishwa mahakamani.

“Wizi wa mitihani ni kosa la kimaadili, tukikukamata, mbali ya kukupeleka tume ya walimu kwa shauri la kiusuluhishi, hatutaishia hapo, tutahakikisha mbali ya kufukuzwa kazi tutakupeleka mahakamani na hatimaye ufungwe jela” alisema Nzunda.

Awali akitoa maelezo na malengo ya mafunzo, Mwakilishi kutoka Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za Umma PS3 anayeshughulikia Rasilimali watu Geoffrey Lufumbi, alisema katika utafiti uliofanyika kuhusu OPRAS Mwezi February 2017, ilibainika asilimia 80 ya watumishi waliohojiwa walionesha kutofahamu jinsi ya kuweka malengo sahihi ya utendaji kazi.

“Katika tafiti tendaji tuliofanya kwenye mikoa miwili ya Dodoma na Iringa na Wilaya nne tulibaini kuwa asilimia 40 walikuwa hawajazi kabisa OPRAS, asilimia 75 walisema hawaoni faida ya OPRAS, aidha asilimia 100 ya Wakurugenzi waliohojiwa walisema hawajazi fomu za upimaji kazi uliowazi za OPRAS”. Alisema Lufumbi.

Lufumbi alisema ili mafunzo hayo yawe na tija ameomba Ofisi ya Rais TAMISEMI kupeleka maelekezo maalum kwenye Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ya kwamba  ifikapo tarehe 05 Jamuari, 2019 Wakuu wa Shule za Sekondari na Msingi wawe wamewezeshwa kuwaelekeza walimu namna ya kujaza OPRAS kwa kufuata mwongozo ulioboreshwa.

Serikali ilianzisha matumizi ya mfumo wa upimaji kazi uliowazi na tathmini ya utendaji kazi kupitia waraka namba 2 wa 2004 na kufuta mfumo wa zamani ambao ulikuwa wa siri na wa vificho usiompa fursa mwajiriwa kutathiminiwa kwa uwazi na ambao ulikuwa ukizorotesha uwajibikaji katika utumshi wa umma.

Anaandika  Atley Kuni, OR-TAMISEMI

Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wakati akifungua mafunzo hayo 
ambapo washiriki hao watalazimika kwenda kuwafundisha walio chini yao

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.