• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Mweli ahoji kushuka kwa Kiwango cha Ufaulu Shinyanga

Imewekwa tar.: March 11th, 2020

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulika Elimu OR-TAMISEMI Gerald Mweli amehoji kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa Mkoa wa Shinyanga Kitaifa kutoka nafasi ya 3 kwa mwaka 2018 hadi nafasi ya 13 kwa mwaka 2019.

Akizungumza katika ziara yake ya kikazi Mkoani humo amesema haiwezekani kwa kipindi cha mwaka mmoja Mkoa huo kuporomoka kitaaluma kwa kiwango hicho jambo lililomfanya aanzie ziara yake Mkoani hapo ili kufahamu kulikoni na  namna walivyojipanga kurudi katika nafasi nzuri zaidi kitaifa.

“Akielezea sababu za kuporomoka huko Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Afisa Elimu Mkoa huo Mohamed Kahundi amesema tatizo kubwa lililopo ni uhaba wa walimu haswa wa masomo ya Sayansi, uchakavu wa miundombinu pamoa na hulka ya Mkoa huu wa kupendelea ufugaji hivyo kuhamasisha watoto kwenda kufuga kuliko kuzingatia masomo.

“Tunajitahidi sana katika kuhakikisha tunatoa elimu bora lakini upungufu wa walimu haswa katika masomo ya Sayansi umechangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma jitihada wa kupandisha kiwango cha elimu katika Mkoa huu” alisema Kahundi.

Aidha Kahundi aliongeza kuwa uchakavu wa miundombuni katika baadhi ya shule piani miongoni mwa changamoto zinazoshusha ari ya walimu kufundisha kwa ufanisi lakini pia na wanafunzi kutokufanya vizuri katika masomo yao.

Akizungumzia hulka ya kupenda kuchunga kuliko masomo amesema wazazi wa Mkoa huu haswa ameneo ya pembezoni hupendelea kuwapeleka watoto machungani lakini sio kumshawishi mtoto kutumia muda wake wa mapumziko kujisomea hivi vyote kwa ujumla vimechangia katika kushusha kiwango chetu cha Elimu kwa kipindi husika alisisitiza Kahundi.

Naibu Katibu Mkuu Mweli amesema haoni kama sababu zilizoainishwa zinaweza kuchangia moja kwa moja kushusha kiwango cha Elimu kwa sababu changamoto hizo sio ngeni katika mazingira yao na ilikuwaje katika mwaka 2018 kufanya vizuri na mwaka uliofutia kufanya kushuka je ni kwamba changamoto hizo zimetokea baada ya mwaka huo au zilikuwepo kwa kipindi chote.

“Nimezipoeka lakini hazijanishawishi na inabidi kushughulikia kila moja kwa namna yake kama ni ya miundombinu ishughulikiwe kimiundombinu na kama ni ya Kitaalumu halkadhalika nayo iweze kushughulikiwa kitaaluma” alisema Mweli.

Kwa sasa hivi tunarekebisha miundombinu katika shule nyingi Nchini kupitia mradi wa Lipa kulingana na matokeo(Paying for Result – Ep4r), shule nyingi sana Nchini tumeshazifikia na kupitia ziara hii pia tumekuja kuona uchakavu wa shule za Mkoa huu ila nazo ziweze kufanyiwa marekebisho hivyo hili sasa litakwisha na sitarajii kuliskia tena kama changamoto alisisiza.

Aliongeza kuwa changamoto iliyoibaini kutokana na taarifa hiyo ni usimamizi; Nina mashaka na usimamizi kuanzia kwenye Waratibu wa Elimu Kata, Walimu Wakuu, Walimu wa Taaluma pamoja na walimu katika kufundisha vipindi ipasavyo.

Suala la upungufu wa walimu sioni kama ni changamoto katika Mkoa huu maana walimu wa masomo ya sanaa takwimu zinaonyesha wapo wa kutosha je hawa wanafanya kazi ipasavyo kabla hamjaanza kuomba hao walimu wa Sayansi tunataka kuona hawa waliopo wamefanya kazi kwa kiasi gani na imeleta matokeo chanya kwa kiwango gani alihoji Mweli.

Hivyo tuongeze nguvu katika ksuimamia katika ngazi ili kila mtu atimizie wajibu wake nina uhakika mtarudi kwenye kiwango kile au hata na zaidi kwa sababu tayari mlionyesha mnaweza na nitapenda kuona mafanikio yale ya mwaka 2018 yanafikiwa.


Naibu Katibu Mweli katika ziara yake Mkoani Shinyanga mefanya kikao na wasimamizi wa Elimu sambamba na kutembelea shule ya ufundi Mwadui , shule mpya ya wasichana inayoendelea kujengwa hapo hapo Mwadui zote zipo katika Halmashauri ya Kishapu kuangalia uchakavu wa miundombinu na namna Serikali inavyoweza kuchukua hatua za makusudi za ukarabati ili kuboresha utoaji wa Elimu.

Kupitia ziara hiyo pia Mweli atatembelea Mkoa wa Geita, Mwanza pamoja na Simiyu.

Mwisho.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha nusu Mwaka (Julai – Disemba, 2019) kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 February 09, 2020
  • Tangazo la kazi kada ya Afya January 20, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • “PS3 plus” Yarudi kwa kishindo, Bilioni 114 kuwezesha Mifumo Sekta ya umma nchini

    January 16, 2021
  • Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

    January 14, 2021
  • Mweli awatolea uvivu kidato cha Nne, Sita, awajenga kinidhamu

    January 11, 2021
  • Mweli awatega Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu kwenye Mfumo wa PREM/PREMS.

    January 10, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.