• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Mifumo ya ukusanyaji wa taarifa za Ustawi wa Jamii yatakiwa kuungana

Imewekwa tar.: January 28th, 2019

Mkurugenzi Msaidizi  wa Huduma za Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais Tamisemi, Rasheed Maftah ameitaka mifumo inayokusanya taarifa za  taarifa za ustawi wa jamii katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa kuungana na kuwa  mfumo mmoja unaotoa taaarifa zote zinazohitajika katika kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Maftah ameyasema hayo wakati wa kikao maalum cha kuwapitisha wataalamu na wadau kwenye mfumo wa Ustawi wa Jamii wa taarifa za watoto walio katika mazingira hatarishi (MVC-MIS) unaowezeshwa na Taasisi ya MEASURE Evaluation; Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Reform OR-TAMISEMI mwishoni mwa juma lililopita.

Kupitia kikao hicho  wataalamu wa mifumo hiyo  waliweza kuwapitisha wadau kwenye mfumo unaoenda sanjari na MVC-MIS ambao ni USSD unaowezeshwa na Taasisi ya pact kizazi kipya.

Maftah alisema ni wakati sasa waataalamu wetu kukutana pamoja na kuona namna gani mifumo hiyo ambayo inakusanya taarifa za ustawi wa jamii kuungana na kuwa na mfumo mmoja ambao utafanya kazi zote zinafanywa na mifumo hiyo kwa sasa.

Aliongeza kuwa kazi hiyo ni lazima ifanywe na wataalamu wa mifumo toka Ofisi ya Rais –TAMISEMI pamoja na Wizara ya Afya wakishirikiana na wale waliotenegneza mifumo hiyo hapo awali kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Measure Evaluation pamoja na Path Kizazi Kipya.

“Ni wakati sasa wa wataalamu wetu kujengewa uwezo na kuifahamu mifumo hii kwa undani na kushiriki katika kuiunganisha ili hapo baadae miradi itakapomaliza muda wake na kuikabidhi mifumo hiyo kwa Serikali tuwe na wataalamu watakaoweza kuindeleza na kuisimamia wadau wetu wanavyofanya sasa” alisema Maftaha.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma toka Ofisi ya Rais TAMISEMI Angelista Kihaga akichangia wakati wa kikao hicho alisema hata kama mifumo hii inawezeshwa na wafadhili lazima waangalie uwezekano wa kuwajengea uwezo zaidi watumishi wa Serikali  ambao wataendelea kuihudumia mifumo baada ya mradi kwisha  kuliko kuajiri watumishi wa muda au kuwajengea uwezo wataalamu wa kujitolea “Volunteers” ambao huondoka mara tu mradi unapomaliza muda wake.

“Sisi kama Serikali lazima tuangalie namna ambavyo mifumo hii inakua endelevu na sio siku  wadau  wakitukabidhi mifumo baasi ndio inakua mwisho wa matumizi ya mifumo hiyo sio sawa; Imefika wakati  ambapo  wataalamu wanatakiwa kufahamu kila kitu katika  mifumo hii ili waweze kuiendeleza hapo baadae” alisema Kihaga.

Awali akiwapitisha wataalam katika Mfumo wa MVC-MIS   Bi. Immaculate Ayebazibwe  Kutoka MEASURE Evaluation alisema kuwa mfumo wa MVC-MIS unawezesha ukusanyaji wa takwimu sahihi zinazofanikisha  upatikanaji wa taarifa za utawi wa jamii, na pia unafanya uchambuzi wa kina wa tawkimu hizo.

Naye Mtaalamu kutoka Pact Kizazi Kipya Bw. Tumaini Mbwambo ambao anasimamia  mfumo wa USSD wa kukusanya taarifa za ustawi wa jamii alisema kuwa mfumo wao unakusanya zaidi  taarifa binafsi  tofauti na ule wa MVC-MIS unaokusanya taarifa kwa makundi.

Wakati huo huo mtaalamu kutoka TASAF Bw. Sesil Latemba alipata furasa ya kuwapitisha wajumbe kwenye mfumo unaotumiwa na TASAF katika kukusanya taarifa za Kaya Masikini kuomba kikao hicho kuona uwezekano wa kuunganisha  mfumo huo na ule wa usatwi wa jamii.

Mfumo huu wa kielektroniki wa  ukusanyaji wa taarifa za watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi wa MVC-MIS unatumika katika halmashauri 67 Nchini na hivi karibuni utafikishwa kwenye halmashauri 106.

Mfumo huu umekuja kuhuisha  ile njia ya awali ya kutumia regista Namba 1 ambayo hutumika kuorodhesha majina ya watoto wote wanaoishi kwenye mazingira hatarishi  katika kijiji au mtaa husika ambao kwa kila mdau anayehitaji kusaidia watoto hao inamlazimu kupitia regista hiyo kuona majina ya watoto wanaohitaji msaada wa kiustawi.


Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Bil 16.4/- zarejesha hadhi ya Shule za Sekondari za Ufundi nchini

    January 22, 2021
  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.