• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Jafo apiga marufuku Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwaswekwa ndani Madaktari

Imewekwa tar.: October 26th, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewataka Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuacha tabia ya kuwasweka ndani madaktari bila ya kufanya tathmini ya makosa waliyoyafanya.

Akifunga Mkutano wa hamsini wa taaluma wa Chama cha Madaktari Tanzania leo jijini Dodoma Mhe. Jafo amesema kuwa kitendo hicho kinadhalilisha taaluma ya udaktari na kuwavunja moyo watumishi hao katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Alisema kuwa kama daktari ana tuhuma yoyote inayomkabili iundwe tume ya kuchunguza makosa hayo kabla ya kumsweka ndani.

Waziri Jafo alifafanua kuwa baadhi ya vifo vinavyotokea hospitalini husababishwa na jamii kwa kuwachelewesha wagonjwa hospitalini lakini pindi kifo kikitokea tuhuma hizo hupelekewa daktari aliyemhudumia.

“Inasikitisha kuona baadhi ya wana familia wanamchelewesha mama mjamzito au mama mjamzito mwenyewe hajahudhuria kiliniki hata mara moja lakini kifo kikitokea daktari anawekwa ndani, hii si sahihi kabisa,” alisema.

Hivyo Waziri Jafo aliwaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuacha mara moja tabia hiyo ya kuwadhalilisha madaktari kwa makosa ambayo pengine siyo ya kwao.

Hata hivyo Mhe.jafo aliwataka madaktari hao  kufanya kazi kwa weledi na kwa ufanisi katika kutoa huduma kwa jamii ili  kuacha alama katika maeneo yao wanayofanyia kazi.

Alisema kuwa taaluma ya udaktari ni muhimu katika jamii kwani husaidia kuokoa maisha ya watu hasa masikini hivyo ni vyema watendaji hao wakatumia taaluma yao vizuri ili waweze kukumbukwa na jamii kutokana na kazi nzuri walizozifanya.

Kwa upande wake Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt Obadiah Nyongole alisema kuwa mkutano huo unalenga kuwaleta pamoja wana taaluma ya udaktari ili waweze kujadiliana miiko na maadili ya taaluma ya udaktari na changamoto zake.

Aliongeza kuwa katika mkutano huo, madaktari walijadiliana namna bora ya kuwafikia wanyonge kwa kuangalia uwezekano wa kuanzisha huduma tembezi za afya hasa maeneo ya vijijini.

Naye Mkurugenzi wa huduma za afya, Ustawi wa jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt Ntuli Kapologwe alisema kuwa Serikali kwa kutambua umuhimu wa taaluma hiyo imejenga nyumba 310 za kuishi za Madaktari katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Alisema kuwa japokuwa nyumba hizo hazitoshi kulingana na mahitaji lakini serikali inafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kuwa inaboresha maslahi ya madaktari ili waweze kufanya kazi zao vizuri za kuwahudumia wananchi.


Na. Angela Msimbira

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.