• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Halmashauri igeni Mfano wa Jiji la Dodoma

Imewekwa tar.: May 24th, 2019

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amezitaka halmashauri zote nchini kuiga mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika utoaji wa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye walemavu.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya mfano yenye thamani ya zaidi ya shilingi bil 1.06 (1,062,500,000) kutoka katika mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa Fedha 2018/19 kwa vikundi 201.

Alisema kuwa halmashauri zingine zihakikishe kuwa asilimia 10 ya mapato yao ya ndani inapelekwa moja kwa moja kwenye vikundi vya wanawake na vijana na watu wenye ulemavu ili kuwainua kiuchumi.

“ Jiji la Dodoma limekuwa la mfano katika mambo mengi kuanzia ukusanyaji wa mapato wameongoza katika pato ghafi na leo hii wametekeleza kwa vitendo Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa Sura Na, 290 kifungu 37A na kanuni zake za utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu za mwaka 2019.

Jafo aliongeza: “ Kukusanya mapato ni jambo moja na utoai wa mikopo ni jambo jingine, halmashauri inaweza kukusanya lakini isitoe mikopo hii kwa vikundi, sasa Dodoma wameyafanya yote haya kwa umakini na ufanisi mkubwa niwapongeze Jiji la Dodoma na niwatake Halmashauri zingine waje kujifunza na kuiga mfano wenu mnafanya kazi nzuri.

Wakati huo huo, Jafo ameutaka uongozi wa Jiji la Dodoma kukaa pamoja na wadau kubuni na kuunzisha mradi mkubwa ambao utaweza kuwanufaisha makundi maalumu ambao utatekelezwa na asimilia 10 ya mapato ya ndani.

“Unajua wananchi wetu wanataka kufanikiwa katika biashara na pia wanapendelea biashara kubwa hivyo mkibuni mradi mkawatengenezea vizuri kisha mkawakabidhi kama sehemu ya mkopo itawajenga na kubadilisha maisha yao kuliko kila siku kuwapa fedha ni vyema wakati mwingine mkawapa vitega uchumi,” aliongeza Jafo.

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe amesema Jiji la Dodoma pamoja na kutoa mikopo hii wameenda mbali zaidi kwa kuhakikisha wanatafuta vyuo vya kutoa ujuzi na maarifa zaidi kwa wanufaika wa Mikopo ili iweze kuwa na tija zaidi.

Pia alisema katika siku zijazo wanatarajia kutoa vifaa na vitendea kazi vya biashara zao kuliko kuwapa fedha ili kuwaepusha na vishawishi vinavyoweza kutokea kutokana na kushika fedha mkononi.

Naye Mkurugenzi wa Jiji hilo, Godwin Kunambi alisema kuwa Jiji la Dodoma limeanza kutoa mikopo kwa vikundi kuanzia mwaka wa fedha wa 2015/16 hadi Desemba 2018 ambapo jumla ya shilingi 2,434,757,316 ziko kwenye mzunguko wa mikopo ya vikundi.

Aliongeza kuwa kiasi cha zaidi ya Sh bilioni 2.6 (2,606,645,760) zilitengwa kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19 huku kiasi cha shilingi 1,796,730,000 kimeshatolea katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2018.

“Fedha za vikundi unazokabidhi leo kiasi cha shilingi 1,062,500,000 zinaifanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2018/19 kutoa mikopo ya jumla ya shilingi 2,859,230,000 sawa na asilimia 109.6 ya malengo tuliyojiwekea” alisema Kunambi.

Jumla ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyokwishanufaika na mikopo ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuanzia mwaka 2015/16 mpaka sasa ni 1,020 vyenye jumla ya Wanachama 10,200 vikiwa na mzunguko wa jumla ya shilingi 3,497,257,316.


Matangazo

  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha nusu Mwaka (Julai – Disemba, 2019) kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 February 09, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • “PS3 plus” Yarudi kwa kishindo, Bilioni 114 kuwezesha Mifumo Sekta ya umma nchini

    January 16, 2021
  • Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

    January 14, 2021
  • Mweli awatolea uvivu kidato cha Nne, Sita, awajenga kinidhamu

    January 11, 2021
  • Mweli awatega Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu kwenye Mfumo wa PREM/PREMS.

    January 10, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.