• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Halmashauri 45 zapewa siku 5 kutoa maelezo ya kutoanzisha Kamati za Watu wenye Ulemavu

Imewekwa tar.: November 26th, 2020

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Dorothy Gwajima amezitaka Halmashauri 45 ambazo hazijaunda kamati za watu wenye ulemavu kutoa maelezo ndani ya siku tano.

Akifungua Mkutano wa wadau wa Chama cha Wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na migongo wazi leo amesema hadi sasa halmashauri 140 zimeunda kamati hizo lakini nyingine bado hazijafanya hivyo, jambo ambalo linarudisha nyuma mikakati ya Serikali ya kuwasaidia watu wenye ulemavu.

Amesema kamati hizo ni muhimu kuundwa kwa kuwa zinarahisha mawasiliano kati ya jamii ya watu wenye ulemavu na serikali na kuweka mikakati bora ya jinsi ya kutatua changamoto zao wanazozipitia katika jamii kwa haraka.

“Kwa halmashauri ambazo hazijaunda kamati hizo natoa siku tano kutoa maelezo wanataka nini ili waunde kamati hizo,waliambiwa mwaka gani na sababu za kutokuunda kamati ni nini na wana mikakati gani ya kuanzisha kamati hizo”, ameagiza Dkt. Gwajima.

Hata hivyo Dkt. Gwajima amesema kuwa kutokuundwa kwa kamati hizo kumesababisha kukata mawasiliano kati ya jamii ya watu wenye ulemavu na Serikali katika suala zima la utoaji wa huduma za afya kwa jamii kwa kuwa lengo la serikali ni kuwafikia watu wenye uhitaji.

Aidha Dkt. Gwajima amewataka wadau mbalimbali nchini kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora kabla ya Ujauzito ili kupunguza tatizo la watoto wenye mgongo wazi  na vichwa vikubwa nchini.

Dkt. Gwajima amesema kuwa kuna umuhimu wa kuweka mikakati itakayosaidia kutoa elimu kuanzia ngazi ya chini ili kujenga uelewa wa pamoja kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa jamii, jambo ambalo litasaidia kumaliza au kupumguza kabisa tatizo la kupata watoto wenye vichwa vikubwa na migongo wazi.

Dkt. Gwajima amesema Serikali imeendelea kuweka mikakati ya kuboresha huduma kwa kujenga na kukarabati vituo vya afya nchini na kupeleka vifaa tiba kwa lengo la kuhakikisha huduma bora za afya zinatolewa kwa wananchi.

Hivyo Dkt.Gwajima ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanatumia vituo vya afya hasa kwa wale watoto wenye matatizo  ya mgongo wazi na vichwa vikubwa.

Pia ameitaka jamii kuacha mila potofu za kuamini kuwa mtoto anapozaliwa na tatizo la Mgongo wazi na kichwa kikubwa kuwa wamelogwa hivyo kupelekea baadhi ya wazazi kuwaficha watoto wao jambo ambalo linasababisha ucheleweshwa kwa matibabu ambayo yangemsaidia kupona kwa haraka.

“Jamii ielimishwe kuhusu chanzo cha kuzaliwa kwa watoto wenye migongo wazi na vichwa vikubwa ili waondokane na dhana potofu walizonazo ili kuwaokoa watoto wenye tatizo hilo na jinsi ya kukabiliana nalo” amesisitiza Dkt. Gwajima.

Dkt. Gwajima ameagiza wadau wote kuhakikisha wanatoa elimu kwa kamati za vituo vya afya nchini kwa kuwa zina wananchi ambao ni wajumbe ili wajue takwimu sahihi ya watoto wenye vichwa vikubwa.

“Wekeni mikakati ya kutumia mifumo ya afya iliyopo katika jamii ili kupunguza watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi katika jamii yetu”, ameeleza Dkt. Gwajima.






Matangazo

  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kipindi cha nusu Mwaka (Julai – Disemba, 2019) kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 February 09, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Viongozi TBA Kigoma matatani kwa kushindwa kukamilisha miradi

    January 18, 2021
  • “PS3 plus” Yarudi kwa kishindo, Bilioni 114 kuwezesha Mifumo Sekta ya umma nchini

    January 16, 2021
  • Serikali yagawa vifaa vya bilioni 3 kwa Wanafunzi 18,488 wenye mahitaji maalum

    January 14, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.