• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Dkt. Gwajima Awaasa Watumishi Kuzingatia Sera ya Ugatuaji katika kazi zao

Imewekwa tar.: January 10th, 2019

Watumishi wametakiwa kuwa na uelewa wa kazi wanazofanya kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa ili kuimarisha uratibu mzuri, uwazi, utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kufanya watanzania wajivunie uwepo wao katika nafasi hizo.

Hayo yamebainishwa leo na Naibu Katibu Mkuu (Afya) Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt.Dorothy Gwajima wakati wa kikao chake cha kwanza baada ya mapokezi yaliyohudhuriwa na menejimenti na watumishi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI jijini Dodoma leo.

“Sisi watumishi ndio ramani ya watanzania kuweza kufikia chachu ya maendeleo ya nchii hii, hivyo tukiratibu na kutekeleza majukumu yetu kwa ufasaha ni haki yetu kupata matokeo chanya ya maendeleo ya nchi hii” Amesema Dkt.Gwajima.

Dkt.Gwajima amesema lazima serikali ijenge mfumo mzuri wa uratibu na utekelezaji wa majukumu yake kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa kwani ndio njia stahiki ya kuweza kupata Tanzania yenye maendeleo na kufanya watanzania kujifunia Utanzania wao.

Akiongea katika kikao cha menejimenti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu (Afya) Dorothy Gwajima, Kaimu Katibu Mkuu Tixson Nzunda Ofisi ya Rais - TAMISEMI), amesema ili mtumishi wa Umma aweze kutimiza majukumu yake ya kila siku ni lazima atambue kuwa yeye ni wakili wa anaowahudumia, mratibu wa matokeo chanya, awe mcheshi kwa jamii anayoihudumia na yeye ajihisi ni sehemu moja wapo ya jamii hiyo.

Katika hatua nyingine kwenye kikao maalum na watumishi wa Idara ya Afya, Dkt. Gwajima amewaasa watumishi wa Idara ya Afya Ofisi ya Rais -TAMISEMI kuuvaa uhusika wa jamii wanayoitumikia katika kutekeleza majukumu yao ili kupata chachu ya kufanya kazi kwa ufanisi, juhudi na kutoa huduma bora kwa watanzania.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe amempongeza Dkt. Gwajima kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo kwa niaba ya Idara yake ambapo ameahidi watampa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora za afya kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa na kwamba wapo tayari kupokea maelekezo yote ya Serikali.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ukaguzi na Ufuatiliaji wa Fedha katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa OR-TAMISEMI Miriam Mmbaga amesema kuwa ameguswa na mfumo aliokuja nao Dkt. Gwajima wa kutaka uratibu, uwazi, utekelezaji na ugatuzi wa madaraka kuanzia ngazi ya kijiji mpaka Taifa na kwamba utaleta chachu ya matokeo bora katika kutekeleza majukumu yao.

Dkt.Gwajima ameteuliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapo jana kuwa Naibu Katibu Mkuu (Afya) Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

                                Anaandika Majid Abdulkarim na Fred Kibano


Matangazo

  • Badili Tahasusi kwa Wanafunzi Kidato cha Tano Tarajali na Vyuo vya Kati March 29, 2021
  • Kitabu cha Maombolezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mhe. John Pombe Joseph Magufuli March 18, 2021
  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • TARURA Iringa watumia shilingi milioni 153 kukarabati barabara za Kalenga

    April 12, 2021
  • Shilingi bilioni 1.5 zatumika kujenga vituo vinne vya afya Tunduru

    April 12, 2021
  • Waziri Ummy aanza na Sekretarieti za Mikoa

    April 12, 2021
  • Katibu Mkuu mpya Ofisi ya Rais TAMISEMI akabidhiwa ofisi

    April 12, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.